Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Saturday, March 26, 2011

Maandamano makali Yemen




Mamia kwa maelfu ya watu walitazamiwa kushiriki maandamano makubwa katikati ya mji mkuu wa Yemen, Sanaa wiki moja baada ya watu hamsini kuuawa na vikosi vya usalama wakati wakiandamana.


Waandamanaji walikuwa wamepanga maandamano makubwa kuwahi kufanyika ya kudai Rais Ali Abdullah Saleh ajiuzulu.




Bw Saleh ameuambia mkutano wa halaiki ya wafuasi wake kuwa yuko tayari kuachia madaraka, ila tu kwa mtu anayemuamini.

Askari walifyatua risasi angani kuwazuia wafuasi wa Bw Saleh wasielekee waliko waandamanaji wanaompinga kiongozi wao.

Katika hotuba yake, Rais Saleh ambaye amekuwa madarakani kwa zaidi ya miongo mitatu ameshutumu mauaji ingawa aliwataka wafuasi wake wawe na msimamo imara.

Kabla ya hotuba hiyo alikanusha kuwa alihusika kwa vyovyote vile katika mauaji ya waandamanaji wiki iliyopita.

Shirika la Amnesty International limeionya serikali dhidi ya matumizi ya nguvu ya kupindukia, na kuongezea kuwa serikali haiwezi kutumia risasi kutanzua mgogoro unaoikabili.








Maadui Libya wavaana miji muhimu




Walioshuhudia wamesema waasi wa Libya wanakaribia kupambana na majeshi yanayomtii Kanali Gaddafi kwenye mji wa Ajdabiya.

Ndege za Ufaransa na Uingereza zimerusha mabomu karibu na mji ulio mashariki mwa nchi hiyo wakati wa usiku, yakiwemo makombora ya serikali.


Libya
Waasi walijaribu kuwashambulia wanajeshi wanaomwuunga mkono Gaddafi baada ya kufanyika mashambulio ya ndege, lakini walisema ilibidi waghairi.


Mji huo umezingirwa kwa siku kadhaa sasa. Wakazi waliokimbia walisema mitaa ilibaki mitupu, na majeshi ya serikali yalikuwa yakifyatua risasi kiholela.


Majeshi ya nchi za magharibi yalianza kushambulia kwa mabomu wiki iliyopita kwa nia ya kutekeleza azimio la Umoja wa Mataifa lililozuia majeshi ya Libya kuwashambulia raia kwa ndege.


Majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya, Nato yanatarajiwa kuongoza harakati hizo za kijeshi badala ya Marekani kwa siku zijazo.








Maafisa wamesema uvamizi huo umedhoofisha majeshi yanayomwuunga mkono Gaddafi kwa kiwango kikubwa, lakini mapigano yameendelea Misrata kwa upande wa magharibi na Adjabiya huko mashariki.

No comments:

Post a Comment