Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Saturday, February 19, 2011

Waathirika wa mabomu kufidiwa Tanzania

Nyumba iliyoporomoka baada ya mlipuko
Wakati wakazi wa jiji la Dar es salaam wakiendelea kutafakari juu ya milipuko ya mabomu katika kambi ya kijeshi ya Gongo la Mboto na athari zake kwa maisha ya watu na mali, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ametoa taarifa maalum kuhusu maafa hayo.

Taarifa hiyo ilijaa ahadi za serikali kuwasaidia waathirika wa milipuko hiyo pamoja na ndugu wa watu waliofariki dunia kwa kuwapatia fidia

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari amelielezea tukio hilo kuwa maafa makubwa kwa taifa kutokana na watu kupoteza maisha na mali zao na pia jeshi kupoteza hazina yake ya silaha baada ya maghala 23 kuteketezwa na moto.

Serikali imetangaza kugharamia mazishi ya marehemu popote ndugu zao watakapoamua wakazikwe na baadaye ndugu hao wa marehemu watapatiwa kifuta machozi ambacho hata hivyo hikijatamkwa bayana ni kiasi gani.


Mlipuko Dar es Salaam
Rais Kikwete ambaye ametembelea eneo la tukio na kuwafariji majeruhi wa ajali hiyo katika hospitali mbalimbali za Dar es Salaam walikolazwa,
amesema serikali pia itagharamia matibabu yao na watakaporuhusiwa kutoka hospitali, nao watalipwa kifuta machozi kwa ulemavu walioupata,
ambapo baadhi yao wamepoteza viungo vya miili yao ikiwemo mikono na miguu.

Taarifa hiyo pia imeviagiza vyombo husika kuwahudumia wananchi waliopoteza makaazi yao na waliolazimika kuyakimbia kwa nia ya kuokoa maisha yao kwa kuwapatia haraka makazi ya muda na huduma za malazi, chakula, maji, afya na usafi wa mazingira.

Pia vyombo husika vimeagizwa kuzitambua mapema nyumba, wenye nyumba na kuhakikisha matayarisho na tathmini vinafanyika ili watu hao walipwe fidia inayostahili bila kuchelewa.

Ahadi kama hii ya serikali pia ilitolewa mwaka 2009 baada ya milipuko ya mabomu ya Mbagala,
lakini wengi wa waathirika walilamikia kukosa msaada huo kutokana na usimamizi mbovu,

ambapo wengi walilalamikia upendeleo katika tathmini hususan ya nyumba zilizoharibiwa na kuambulia kupata kiasi kisichokidhi ujenzi mpya wa nyumba zao.


Milipuko ya Gongo la Mboto imesababisha vifo vya watu 20 na mamia wengine kujeruhiwa, huku uharibifu mkubwa wa mali ukionekana.















Wednesday, February 16, 2011

Ruksa Wanaume Kuwaoa Wanaume Wenzao Kanisani


Serikali ya nchini Uingereza inapitisha sheria wiki hii ambayo itabadili maana halisi ya ndoa na kufanunua kuwa ndoa si lazima iwe ni mwanamke na mwanaume bali watu wa jinsia moja nao wanaweza kuoana na pia ndoa zao kufungwa kanisani.
Watu wa jinsia moja wataweza kufunga ndoa kanisani kwa mujibu wa sheria mpya zinazotarajiwa kutangazwa wiki hii nchini Uingereza.

Mashoga na wasagaji wataweza kufunga ndoa kanisani na sherehe zao zitaongozwa na wachungaji na viongozi wengine wa dini.

Mbali ya ruhusa hiyo, serikali ya Uingereza ina mpango wa kuibadili maana ya ndoa katika katiba ambapo ndoa ilikuwa ikijulikana kuwa ni kati ya watu wa jinsia mbili tofauti, mwanamke na mwanaume.

Sheria hiyo mpya itawawezesha wanaume kuwaita wanaume wenzao "Mume wangu" au "Mke wangu" hali kadhalika kwa wanawake nao wataweza kuitana mume na mke.

Kanisa la Anglikana limesema kuwa litakubalina na sheria hiyo na liko tayari kuruhusu majengo ya makanisa yake kutumika kuwafungisha ndoa mashoga na wasagaji.

Hata hivyo kanisa la Church of England limetangaza kuwa halitaruhusu ndoa kama hizo kufanyika kwenye makanisa yao.

Chama cha siasa cha Liberal Democrats ndicho kilichoipigia kampeni sheria hiyo ili kutimiza ahadi za usawa walizozitoa wakati wa kampeni ambazo ziliwafanya wapate kura nyingi kiasi cha kuweza kuunda serikali ya mseto na chama cha Conservative Party.

Jumuiya za kiislamu na jumuiya za kanisa katoliki zimeendelea kusisitiza kuwa mafundisho yao yanasema kuwa ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke.



EU yaitaka Libya isiwabane waandamanaji





Umoja wa Ulaya umeutaka uongozi wa Libya kuwaruhusu raia wake kujieleza kwa uhuru baada ya machafuko ya jana usiku yaliyotokea mjini Benghazi na kutangazwa na vyombo vya habari nchini humo.Kulingana na taarifa za kituo cha televisheni cha taifa,kundi la kiasi ya watu 500 waliandamana nje ya afisi za serikali ili kuushinikiza uongozi kumuachia huru mwanaharakati mmoja kabla ya kuelekea kwenye uwanja ulio katikati ya mji mkuu.Duru zinaeleza kuwa purukushani zilitokea pale polisi na wafuasi wa serikali walipopambana na wanaharakati hao.Kwa mujibu wa mkurugenzi wa hospitali moja kwenye eneo hilo,watu 38 wakiwemo maafisa wa polisi walijeruhiwa na wakapewa matibabu kwenye hospitali hiyo.

Wakati huohuo Serikali ya Libya ilitangaza leo kuwa itawaachia huru kutoka gerezani wanaharakati 110 wakiislamu .






MuIraqi aliyetoa taarifa za silaha za maangamizi makubwa ajigamba



Raia mmoja wa Iraq aliyebainika kuwa na nafasi muhimu katika hali iliyochangia kuuhalalisha uvamizi wa Marekani nchini mwake mwaka 2003 anaripotiwa kuwa anajivunia kuwa chanzo cha kuvurugika kwa utawala wa Saddam Hussein.Hii leo,gazeti la Uingereza la,The Guardian-lilichapisha ripoti zinazoeleza kuwa Rafid Ahmed Alwan al-Janabi aliyepewa jina la Curveball na majasusi wa Marekani na Ujerumani waliokuwa wakikichunguza kisa hicho-ndiye aliyeeleza kuwa uongozi wa Saddam Hussein una silaha za maangamizi makubwa.Kulingana na gazeti hilo,Rafid al-Janabi anajigamba kuwa alipata fursa ya kusambaza uvumi uliochangia kuuondoa madarakani uongozi wa Saddam Hussein.Hata hivyo uchunguzi uliofanywa ulibaini kuwa hakukuwweko na silaha zozote za maangamizi nchini Iraq.

Sunday, February 13, 2011

It's kind of cool about 10/10/10 isn't it? Definitely 10:10 (am and pm)


Dear ....

It's kind of cool about 10/10/10 isn't it? Definitely 10:10 (am and pm) would be significant times, and I think that 8:10pm would be also. In 24-hour time that's 20:10...!


Here's what occurs to me as I think about this number: it's all binary, alternating between the poles (like switching between positive and negative poles of a magnet). Another way to think of 1 and 0 in binary terms is 0=off and 1=on. So it would be like turning your lights on and off repeatedly: 101010 (on/off/on/off/on/off -- or FLASH/FLASH/FLASH) This would be like a signal or initiating code, perhaps to dna or other activation. Think of this as binary = polarity.

My younger son (10th grader) told me one (1!) of his teachers pointed out that in binary (ie, Base2 number system): 101010 is equal to 42 in our decimal system. This is true, I checked it out. [Side note: Binary is the basic underlying number system of physical reality: on or off, yes or no, yin or yang, me or not-me -- in other words: DUALITY)

What's VERY interesting about that is relevant if you ever read or watched The Hitchhiker's Guide to the Galaxy (a very famous/popular book from the 1980s that was a BBC series on PBS and recently was made into a movie). The heroes search the galaxy for the answer to the most important question in the universe. After many adventures, they find the computer at the center of the galaxy, and the answer is "42". (with no explanation. In the second series of stories, they search for the question. It's "What is 7x6?")

My point is that 101010 is 42 and therefore is the Answer to the MOST IMPORTANT QUESTION IN THE UNIVERSE!!

Now I just had an additional thought about 42. The first part is a bridge to the deeper thought. 42 is interesting in that if you divide it by 7 (sacred number/divine number -- with both Light and Dark polarities: Seven Sacraments vs Seven Deadly Sins, etc etc), the result is 6. Numerologically 42 = 4+2= 6. So it relates to itself in a fractal way. Another corroboration of this is 101010 = 3 (numerologically), which is half (binary) of 6.

Now another importance of 7x6 is that it represents 6 weeks, also is an approximation of the significant 40 days (e.g., of Lent, of The Flood, of the days in the Desert), so 101010 might be the starting of a 6-week period of reflection and incubation (root of that word is cube, as in the power of 3), at the end of which some significant event will be over (the end of the incubation). I don't know what, but this is the most interesting stream of consciousness writing I have done in a while, and it feels right.

I am looking forward to your feedback and reaction. You will bring a great insight into this!

Happy [dang! I was about to write "Happy 101010 Eve", when I realized the CUBE: it's obvious 10x10x10!!!]

The Ka'aba in Islam is the big cube that Muslims visit on a haj (pilgrimage). It has something to do with a black rock from space (trust me). The word Cube comes from the Arabic Ka'aba. It might also be spelled Qa'aba and many other ways similar. Look for it with black rock (as in the temple of the rock) I'm typing too fast now, getting more thoughts, and I have to leave to pick up my son.

WOW! Thanks for triggering this!

Wednesday, February 9, 2011

Maharamia wateka meli ya Italia

Jeshi la wanamaji la Italia limesema maharamia wamekwea na kuchukua udhibiti wa meli ya mafuta ya Italia katika bahari ya Hindi.


Meli ya Ujerumani ambayo pia imetekwa


Maharamia hao walifyatua risasi katika chombo kiitwacho Savina Caylyn, takriban kilomita 800 kutoka pwani ya Somalia.

Msemaji wa jeshi la wananamaji amesema hakuna aliyejeruhiwa miongoni mwa mabaharia 17 kutoka India na wataliano watano.


Maharama wamejipatia mamilioni ya dola


Msemaji wa jeshi la wanamaji la Umoja wa Ulaya amesema shambulio la chombo hicho limefanyika katika eneo la mashariki mwa kisiwa cha Yemen cha Socotra.

Meli hiyo imebeba shehena ya mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika bandari ya Pasir Gudang nchini Malaysia, limeripoti shirika la habari la Reuters

Wanajeshi wa Marekani wakiwa na maharamia


Meli ya kivita ya Italia ilikuwa ikielekea katika eneo la tukio, lakini iko umbali wa kilomita 600, na inatarajia kuchukua siku kadhaa kuwasili, limeripoti shirika la habari la Italia.

Umoja wa Ulaya umesema meli hiyo imetekwa na mashua moja ikiwa na maharamia watano

Maharamia wa Somalia


Msemaji wa jeshi la wanamaji wa Umoja wa Ulaya amesema meli hiyo "ilikuwa ikielekea magharibi," upande wa pwani ya Somalia, shirika la habari la AFP limekaririwa.

Maharamia wa Kisomali wametjipatia mamilioni ya dola katika miaka ya hivi karibuni kwa kuteka meli za mizigo katika njia inayotumiwa na meli katika pembe ya Afrika.

Tuesday, February 1, 2011

Kashfa nyingine Mwananyamala


VICHANGA 10 wanaodaiwa kufa katika hospitali ya Mwananyamala wamekutwa wamekufukiwa katika shimo la futi moja na nusu kwa pamoja.
Vichanga hivyo vimekutwa vimezikwa maeneo ya Mwananyamala Kwa Msisiri pembezoni mwa makaburi ya Kwa Kopa na tukio hilo kuvuta watu wengi kufika neo hilo kushuhudia tukio hilo.

Vichanga hivyo vimeviringishwa katika shuka moja lenye nembo ya hospitali hiyo na kuzikwa katika shimo moja lenye urefu futi moja na nusu.
Maiti hizo zimekutwa katika eneo la Mwananyamala Msisiri, jijini Dar es Salaam, pembezoni mwa makaburi ya kwa Kopa mita chache kutoka katika hospitali hiyo.

Maiti hizo zilibainika kwenye eneo hilo na mtu mmoja aliyefahmaika wka jina la MBaga alipokuwa akifanya usafi katika eneo hilo majira ya saa 3 asubuhi na kubaini shimo hilo.
Aliona shimo ambalo lilikuwa haliajaa taka na aliposegelea ndipo aliona mkono wa kichanga kimoja na ndipo aliwaita majirani wa karibu kasha kulipoti tukio hilo kituo cha polisi Oysterbay.

Ndipo polisi walipofika eneo hilo wakafukua na kukuta maiti za watoto wachanga 10 na zilikuwa zimeshaharibika na kukatika viungo wakati wanatolewa shimoni humo.

Maiti hizo zilikuwa zimezikwa na plasta zao mikononi zilizoonyesha walikuwa wamtoka katika wodi moja hospitalini

Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alikutana na viongozi wa juu wa wilaya hiyo wakiwemo madaktari waandamizi kwenye ukumbi wa hospitali hiyo kuzungumzia tukio hilo mkutano uliochukua zaidi ya masaa mawili.

Hata hivyo jeshi la polisi mkoani Kinondoni wanafanuya uchunguzi wa kina kufuatia tukio hilo


Hata hivyo haijafahamika mara moja sababu ya vichanga hivyo kuzikwa kwa pamoja bila ya wazazi kujua

Waandamanaji wamepuuza amri ya serikali




Waandamanaji wamepuuza amri ya serikali


Maelfu ya watu wameendelea na maandamano katika mji mkuu wa Misri, Cairo, huku maandamano hayo yakiingia siku ya saba.


Waandamanaji hao wanatoa wito wa kufanyika mgomo wa kitaifa kuanzia hapo kesho Jumanne.

Polisi wameagizwa kurejea kwenye barabara za mji wa Cairo walizoziacha siku ya Ijumaa, wakati yalipofanyika mandamanao makubwa ya kuipinga serikali.

Serikali ya Misri inasema Polisi wameagizwa kushirikiana na Jeshi.

Waandamanaji wanataka Rais Hosni Mubarak aondoke madarakani baada ya kutawala kwa muda wa miaka 30.


Amejaribu kutuliza ghasia kwa kuahidi mabadiliko ya kisiasa, na akamwagiza waziri mkuu mpya Ahmed Shafiq kuharakisha mabadiliko ya kidemokrasia ili kubuni nafasi mpya za kazi.

Lakini waandishi wanasema ishara zote zinaonyesha mabadiliko pekee yatakayokubalika na waandamanaji ni Rais Mubarak kuondoka madarakani.


Mwandishi wa BBC anasema waandamanaji wengi bado wanaghadhabishwa na jaribio la Polisi kutumia nguvu kuzima maandamano.

Waandamanaji hao wameripotiwa kuzidisha harakati zao huku wakitoa wito wa kufanyika mgomo wa kitaifa na maandamanao makubwa mjini Cairo siku ya Jumanne.

Mjini Cairo kwenyewe helikopta za kijeshi zimeendelea kuzunguka angani karibu na bustani ambapo maelfu ya watu walikusanyika licha ya amri ya kutotoka nje usiku iliyotangazwa na serikali.

Jeshi limeripotiwa kuimarisha vituo vya ukaguzi kote mjini Cairo.

Wakati huo huo, Rais wa Misri Hosni Mubarak amefanya mabadiliko zaidi katika serikali yake huku wasi wasi ukiongezeka kuhusu athari za maandamano hayo juu ya uchumi wa nchi.


Taarifa zinasema Rais Mubarak amembadilisha waziri wa fedha Youssef Boutros-Ghali.

Hatua hiyo inakuja baada ya shirika moja la kimataifa la kukadiria uchumi kushusha viwango vya uthabiti wa uchumi wa Misri hadi chini ya sufuri.

Pia kuna taarifa kwamba waziri wa mambo ya ndani Habib al Adly ameondolewa na nafasi hiyo kuwekwa mtu mwingine.

Maelfu ya raia wa kigeni walioko mjini Cairo wanaendelea kusafirishwa kurudishwa makwao.



Raia wa kigeni waliokwama katika uwanja wa ndege Cairo


Kundi la kwanza la raia wa Marekani wanasafirishwa leo kutoka Cairo kupelekwa nchini Cyprus, katika mwanzo wa mpango ulioanzishwa na Marekani.

Uchina, Japan na Australia pia zimetuma ndege kuwachukua raia wao huku kukiwa na taarifa kwamba mamia ya raia wa kigeni wamekwama kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Cairo.

New Zealand imesema huenda ikatumia usafiri wa kijeshi kuwahamisha raia wake kutoka Misri.

Nchi nyingi duniani zimewatahadharisha raia wao dhidi ya kusafiri kwenda Misri








Protests in Egypt are larger and more intense than they’ve ever been before. “Unprecedented” is the word most frequently used to describe the current political events there. The size of the democratic revolt is unprecedented, as are the levels of repression and censorship. After videos like this Tiananmen square incident and this government shooting were posted to internet sites, the Egyptian government shut down Facebook, Youtube, Twitter, and other social networking sites. This extreme form of government repression and censorship reminds me of the Iranian protests after their June 2009 election was allegedly rigged. The main difference between these protests and those of the Green Movement in Iran is that the Egyptian regime is a staunch ally of the US, whereas the Iranian government is Americas top foe in the region. This fact makes for an extremely delicate challenge for the Obama administration.








How should the U.S. respond when a democratic revolution threatens to topple a government that serves our interests?

In his State of the Union, the President spoke of the ideas our nation was founded upon. Perhaps the two most fundamental ideas of the American revolution was that all people have the rights to liberty and to govern their own affairs. The political repression in Egypt is on par with the harshest in the world. The economy has been horribly mismanaged for years. Egyptians don’t have certain inalienable rights. America’s fundamental values from which American exceptionalism is derived – liberty, democracy, and the pursuit of happiness – are in direct conflict with a state which protects our core vital interests i.e. counter-terrorism, cheap flow of oil through the Suez Canal, as well as mediation in regional issues such as Gaza, Lebanon, and Iran. Our values conflict with our realpolitik national interests. Historically, for the United States the later has nearly always trumped the former; our core vital interests as a state override our the values we profess to uphold.


But this is the wrong time to forsake our values. Not only is standing on the side of freedom and democracy the right thing to do, if the calculation of the United States’ core interests is made with a long-term view, it is also in the best interest of the United States. Mubarak is 84 years old and sick, the population is young, unemployed and restless, and inflation is off the charts. These protests may or may not topple the regime, but they have already made the US support for Mubarak more costly. Mubarak’s succession is imminent. One way or another he will be replaced soon. Rather than attempting to prop him (or his son) up indefinitely, the United States should support the people of Egypt, both in words and deeds by using its immense leverage with the Egyptian government to make serious, democratic reforms.

Like all revolutions, the one gathering steam in Egypt is multifarious. Thus, it is difficult to tell whether the next government of Egypt (whenever it comes) will be closer in political outlook to the Muslim Brotherhood or Mohammed El-Baraedi. The US would certainly prefer the later, but that is not a choice for the US to make. Instead it should distance itself from the Mubarak regime (something the Obama administration is already beginning to do). The US should also seek better relations with future power brokers in Egypt, so that when power changes hands the US will be more likely to find common ground with the new regime.

Usingizi relini

Bwana mmoja nchini Japan, baada ya kutoka katika matembezi yake ya usiku ambapo alikuwa amekunywa pombe kikamilifu, alipitiwa na usingizi wakati akirejea nyumbani na kulala juu ya reli.


Reli



Bwana huyo kutoka Chiba Prefecture , mapema wiki hii aliuchapa usingizi kisawasawa katikati ya mataruma ya reli na kuanza kukoroma.

Dereva wa treni ya mizigo iliyokuwa ikipita katika reli hiyo, aliweza kumuona bwana huyo , na mara moja akaweka breki za dharura kuisimamisha treni hiyo iliyokuwa katika mwendo wa kasi.


Kwa bahati mbaya, au nzuri, treni hiyo ilishindwa kabisa kusimama, na kupita juu ya mlevi huyo, ambaye aliendelea kukoroma bila kujua kinachotokea. Baadaye mlevi huyo alishituka, na kukuta behewa la treni limesimama juu yake, na hivyo kulazimika kutambaa na kutoka chini ya treni hiyo.

Mtandao wa habari wa Japanator umesema wachunguzi wanasema, bwana huyo ana bahati kubwa kwani kulikuwa na nafasi ya kutoka kati ya trenni ya reli, la sivyo angesagwasagwa. Tukio hilo lilisababisha kuchelewa kwa treni tatu kwa karibu dakika kumi na nne, na kusababisha usumbufu kwa abiria wapatao mia saba.

Party za Krismasi


Krismasi



Wafanyakazi wengi wanadhani sherehe za kiofisi za Krismasi zitaharibiwa iwapo wakuu wa kazi nao watahudhuria sherehe hizo.


Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa, mbali na wafanyakazi kona kwamba hawataweza kufanya vituko vyao, pia wanakuwa na mashaka ya nguo watakazovaa, ambazo huenda mabosi wao wakawa waharidhiki nazo sana. Utafiti huo umefanywa na mgahawa wa TGIF. Katika watu elfu mbili waliohojiwa, asilimia 27 walisema wana wasiwasi huenda wakashindwa kujizuia kusema jambo ambalo halitamfurahisha mkuu wake wa kazi -- hasa baada ya kuwa wamepata kinywaji.


Wengine hata wamehisi kuwa huenda wakazusha ugomvi wa kurushiana makonde. Robo ya watu hao wamesema kuwepo kwa bosi wao kunapunguza watu kuwa na raha, wakati mmoja kati ya watu watano wamesema ni bora mabosi hao wasihudhurie kabisa sherehe hizo.

Asilimia moja ya watu hao wamesema walilazimika kuacha kazi baada ya party hizo za kiofisi za mwisho wa mwaka. Mkurugenzi wa mauzo wa TGIF Darrel wade amesema "sherehe za kiofisi za Krismasi ni watu kufurahia na kusherekea kwa kazi walizofanywa kwa mwaka mzima.-- Mabosi wanaotaka kwenda katika sherehe hizo, wanatakiwa wawaachie huru wafanyakazi wao."