Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Friday, April 29, 2011

Mwanamfalme wa Uingereza, William na mkewe Kate Middleton wameonekana hadharani



Mwanamfalme wa Uingereza, William na mkewe Kate Middleton wameonekana hadharani kwa mara ya kwanza wakiwa kama wanandoa wapya. Baada ya kuhitimisha ibada ya misa katika Kanisa la Westminster Abbey mbele ya karibu wageni waalikwa 2,000 na watu wengine bilioni mbili waliokuwa wakiangalia harusi hiyo ya kifalme kwa njia ya televisheni, William na Kate pia walipigana busu la kwanza hadharani kama mume na mke, wakiwa kwenye kibaraza cha kasri la malkia la Buckingham.


Kabla ya harusi hiyo mapema leo, Malkia Elizabeth wa Pili, alimpa William cheo cha heshima cha kuwa mtawala wa jimbo la Cambridge. Baada ya harusi, Kate amekuwa rasmi mke wa mtawala wa jimbo la Cambridge. Wanandoa hao walijumuika pamoja na wageni 650 kwa chakula cha mchana na sasa wanasubiri sherehe itakayofanyika usiku ambayo itahudhuriwa na marafiki 300 na wanafamilia




Prince William has to ask Queen Elizabeth for her permission before proposing Kate








Prince William and Kate Middleton announced their engagement on Tuesday Nov. 16, 2010. The wedding date has not been announced yet, but it is expected to take place in the spring or summer of 2011. Prince William’s marriage brings a big cheer to the whole Britain in amid economic woes. The royal wedding will be held on the 30-year anniversary of his parents’ wedding. Below are five wedding traditions in British royal nuptials which will surely become hot topic for upcoming newspaper presses.



Asking the Queen\'s permission

It is the tradition that Prince William has to ask Queen Elizabeth for her permission before proposing Kate. The Royal Marriages Act of 1772 requires all descendants to access the sovereign ruler’s approval for the marriage. The British law prohibits royals from marrying Catholics. Hence, if Kate Middleton were Catholic, William would have to choose either the throne or his love










With Diana\'s ring, William and Kate are engaged







Royal rings are made with a piece of Welsh gold.










Diana\'s impressive wedding dress






Residence



There will be an apartment available for them in the royal residence. However, after the nuptial, William and Kate will return to their home in Wales near William\'s Royal Air Force base. An unusual fact is that William and Kate have lived together long before their marriage ceremony. Whenever William\'s service is over, William and Kate will move to a house in Herefordshire.






Royal wedding between Queen Elizabeth and Prince Phillip in 1947






The wedding location

The wedding location of Kate Middleton and Prince William has not been announced yet. Westmister Abbey is most likely the traditional place. Otherwise, St. Paul’s in London where Prince Charles married Princess Diana and St. Georges Chapel in Windsor would be another choice.

















Mahakama yampunguzia Mbatia ada ya kesi yake






MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imempunguzia Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia na wanachama wawili wa chama hicho, ada ya kuendesha kesi yake dhidi ya Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee.

Katika kesi hiyo, Mbatia ambaye alikuwa mgombea wa kiti hicho, uchaguzi mkuu mwaka jana, alifungua kesi kupinga ushindi wa Mdee.Sheri ya Uchaguzi inamtaka mlalamikaji kuweka mahakamani dhamana ya Sh5 milioni kwa kila mlalamikiwa.

Kwa msingi huo, Mbatia kupitia kwa wakili wake, Mohamed Tibanyendela, aliwasilisha maombi mahakamani hapo akiomba mahakama kumpangia kiwango cha chini itakachoona kinafaa.

Hata hivyo, sheria hiyo pia inatoa nafasi kwa mlalamikaji kuomba kusamehewa au kupangiwa kiwango cha chini zaidi ya hicho kilichotajwa kwa kadri mahakama itakavyoona kulingana na mazingira ya kesi husika.

Lakini, Mbatia aliwasilisha maombi mahakamani hapo kupitia kwa wakili wake, Tibanyendela akiiomba mahakama kumpunguzia kiasi hicho, badala yake alipe Sh1 milioni kwa kila mlalamikiwa.

Katika maombi hayo, licha ya mambo mengine, Mbatia alidai hivi sasa hana uwezo wa kulipa kiasi hicho kwa sababu ametoka kwenye kampeni za uchaguzi huo.

Wanachama wengine wa chama hicho ambao waliomba kuunganishwa na Mbatia kwenye kesi hiyo, Hemed Kanoni na Solomon Lufunda, waliomba mahakama kuwasamehe kulipa kiasi chochote cha dhamana kwa madai kuwa, hawana uwezo huo kwa sababu ni wakulima.

Akitoa uamuzi huo jana, Jaji John Utamwa, alitupilia mbali maombi ya Mbatia kutaka alipe Sh1 milioni kwa kila mlalamikiwa, na walalamikaji wenzao kutokulipa kabisa kwa sababu zao hazina msingi.Jaji Utamwa aliwapunguzia kiwango hicho na kuwataka kulipa Sh3 milioni kwa kila mlalamikiwa wote kwa pamoja.

Kwa uamuzi huo, Mbatia na wenzake wanapaswa kulipa Sh9 milioni kama dhamana ya kesi yao, badala ya Sh15 milioni, ndani ya siku kumi 14 tangu kutolewa kwa uamuzi huo ili kesi iweze kupangiwa siku ya kusikiliza.

Katika kesi hiyo, Mbatia anapinga ushindi wa Mdee, anachodai kuwa Mdee wakati wa kampeni alitoa tuhuma za uongo kwamba Mbatia alikuwa akipewa Sh80 milioni na CCM, mambo ambayo anadai yalimwathiri katika upigaji kura





Burundi kuadhimisha mauaji ya Wahutu




Raia wa Burundi
Nchini Burundi leo April 29 ni kumbukumbu ya mauaji ya maelfu ya raia wa kabila la wahutu waliouliwa na jeshi mwaka 1972.

Mauaji hayo yalifunikwa funikwa na tawala zilizopishana na hivi sasa baada ya mageuzi ya kidemokrasia shirika moja linakutetea haki za jamii limetaka yaliotendeka yote yawekwe wazi na haki itendeke.

Hata hivyo baadhi ya raia wa nchi hiyo wanaunga mkono juhudi za serikali ya kutenga siku ya kumbukumbu ya maujai hayo ili kuna wale wanaopinga wakisema, huenda ikasababisha uhasama kati ya jamii mbali mbali nchini humo








Mchango kwa Ukarabati wa Chernobyl




Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine (kushoto) na Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya Jose Manuel Barroso.Leo mkutano maalum umefunguliwa Kiev mji mkuu wa Ukraine, ukiwa na azma ya kuchanga fedha za kusaidia kukabiliana na madhara ya ajali ya mtambo wa nyuklia wa Chernobyl uliotokea miaka 25 iliyopita.

Umoja wa Ulaya pekee umeahidi kutoa Euro milioni 110 kusaidia kuugubika mtambo huo kwa kuta za zege. Rais wa Ukraine Viktor Yanukovych katika hotuba ya kuufungua mkutano huo mjini Kiev alisema kuwa Chernobyl ni maafa kwa dunia mzima kwa hivyo ulimwengu mzima unapaswa kushirikiana kupambana na janga hilo. Ajali ya kiwango kikubwa kama hicho haiwezi kuachiliwa Ukraine peke yake. Amesema ajali ya hivi karibuni nchini Japan pia imethibitisha kuwa matukio kama hayo ni changamoto kwa binadamu wote.

Kinu cha Chernobyl kilichomiminiwa zege hiyo miaka 25 iliyopita, sasa kina nyufa na matundu na hivyo mionzi ya sumu ya nyuklia inapenya. Ukarabati uliofanywa kati ya mwaka 2004 na 2008 umetumia vyuma kuimarisha baadhi ya kuta zilizogubika kinu hicho. Julia Marositsch anaefanya kazi katika kitengo cha ushirikiano wa kimataifa cha mtambo wa nyuklia wa Chernobyl anasema:

"Vyuma hivyo vitasaidia kuimarisha jengo hilo la zege kwa takriban miaka 15. Kwa hivyo kuna muda wa kufanya ukarabati na kumimina zege jipya ili kuwa na kuta imara zaidi."


Mtambo wa nyuklia wa Chernobyl ulioripuka 26 Aprili, 1986Kazi hiyo ya ukarabati inahitaji muda huo, kwani kazi ya mradi huo mkubwa ni ngumu kuliko vile ilivyotazamiwa kama anavyoeleza Heinz Smital, mtaalamu wa kinga ya mionzi ya nyuklia wa shirika la ulinzi wa mazingira Greenpeace.

"Haiwezekani kufanya kazi juu ya jengo hilo kwani katika sehemu hiyo viwango vya mionzi ya nyuklia ni vikubwa mno."


Gharama za ukarabati zinaongezeka kila mwaka. Kwa hivi sasa, inatathminiwa kuwa kutahitajiwa kiasi cha Euro bilioni 1 nukta 6 - na jumuiya ya kimataifa inatoa msaada - mfadhili mkubwa ni Umoja wa Ulaya. Na msaada huo unahitajiwa, kwani bado kuna hatari kubwa. Inatathminiwa kuwa asilimia 5 tu ya mionzi ya nyuklia ndio iliyotawanyika wakati wa mripuko. Hiyo humaanisha asilimia 95 bado zimo ndani ya mtambo huo. Na taka hizo za nyuklia lazima zizuiliwe ndani kwa njia yo yote ile anasema Heinz Smital wa Greenpeace.







Foleni baada benki kufunguliwa I Coast




Benki Ivory Coast


Maelfu ya raia wa Ivory Coast wamepanga foleni kutoa pesa na kupokea mishahara iliyocheleweshwa kufuatia benki nchini humo kufunguliwa tena baada ya kufungwa kwa wiki 10.

Kufungwa kwa benki hizo kulitokana na jaribio la aliyekuwa Rais Laurent Gbagbo kung'ang'ania madarakani baada ya uchaguzi wenye utata.

Kufunguliwa tena kwa mfumo wa benki ni hatua ya kufufua uchumi wa nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa kakao duniani.

Serikali ya rais mpya Alassane Ouattara imeahidi kulipa mishahara ya miezi miwili kwa sekta za umma.

Raia wa nchi hiyo walitaarifiwa kwa kipindi kifupi juu ya kufungwa kwa benki hizo mwezi Februari, wakiacha maelfu wakihangaika kumudu maisha yao bila mishahara, mafao ya uzeeni na akiba.

Mteja mmoja aliyekuwa kwenye foleni nje ya benki iliyokuwa kwenye mji mkuu Abidjan, alisema alikuwa akisubiri tangu mapema asubuhi kutoa pesa za kutosha kwa ajili ya kulisha familia yake.

Alisema, "Ntaitunza familia yangu iliyoteseka kwa takriban miezi miwili bila ya kuwa na chakula cha kutosha. Ntawatunza watoto na kuhakikisha wanarudi shuleni. "

Sekta ya biashara nayo imekwama kufanya kazi kwa ufanisi na biashara kuu ya kakao, inabaki ikisuasua.

Mwandishi wa BBC John James aliyopo mjini humo, japo vikwazo vimeondolewa, wafanyabiashara wanahitaji akaunti zao za benki kabla ya kulipa ushuru wa forodha





Mapigano yaendelea Misrata





Mji wa Misrata bado umekuwa ukigubikwa na mapigano makali kati ya vikosi vinavyomtii kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi na waasi wanaoudhibiti mji huo.

Miripuko mikubwa na milio ya bunduki imesikika katika uwanja wa ndege. Misrata ni mji wa tatu kwa ukubwa nchini Libya na ndio mji wa magharibi ambao waasi wanajaribu kuutumia kuingia kwenye mji mkuu wa Tripoli.


Wakati huo huo, katika mpaka na Tunisia wanajeshi wanaomuunga mkono Kanali Gaddafi wamerusha makombora na kupambana na vikosi vya Tunisia katika jaribio la kuwaondoa waasi ambao wamekimbilia kwenye eneo la Dehiba.












Waandamanaji Syria wadai uhuru zaidi








Vyombo vya habari vya Syria vimeripoti kuwa wanajeshi wanne wameuawa na wengine wawili wametekwa na watu wanaojiita magaidi wenye silaha. Shambulio hilo limetokea kwenye mji wa kusini wa Daraa, ambako maelfu ya wananchi


wamekusanyika kudai uhuru zaidi wa kisiasa na kupuuzia umwagaji damu na ukandamizaji unaofanywa na serikali dhidi ya maandamano ya kuupinga utawala wa Rais Bashar al-Assad.


Wanaharakati na kundi la Udugu wa Kiislamu, Muslim Brotherhood, lililopigwa marufuku nchini Syria, waliwataka raia wa nchi hiyo kuingia mitaani katika siku ya ghadhabu baada ya sala ya Ijumaa,

lakini wizara ya mambo ya ndani imesema raia hawatakiwi kuandamana bila kibali. Kundi la kutetea haki za binaadamu limesema matumizi ya nguvu yaliyofanywa na serikali ya Syria yamesababisha mauaji ya watu 500 tangu maandamano yaanze katikati ya mwezi Machi.

Baadae leo wanadiplomasia kutoka serikali za Umoja wa Ulaya watakutana mjini Brussels kujadili uwezekano wa kuiwekea Syria vikwazo. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle, anashinikiza vikwazo dhidi ya Syria na kutaka hatua ngumu za kidiplomasia zichukuliwe.

No comments:

Post a Comment