Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Friday, April 15, 2011

Lazima Gaddafi aondoke, viongozi wasisitiza




Viongozi wa Marekani, Uingereza na Ufaransa wamesema katika ujumbe wa pamoja kwamba hakutakua na amani nchini Libya iwapo Muammar Gaddafi ataendelea kuwepo madarakani.

Shirika la Nato na washirika wake,wanasema, lazima waendeleze harakati za kijeshi ili kulinda raia na kuongeza shinikizo kwa serikali ya Kanali Gaddafi.

Kumuachia aendelee kukaa madarakani,wanasema,itakuwa ni usaliti kwa watu wa Libya.

Nato imekuwa katika harakati za kuongeza ndege zaidi za kijeshi kwa ajili ya mpango huo.

Ni wachache kati ya wanachama wake 28 - ikiwemo Ufaransa,Uingereza, Canada,Ubelgiji, Norway na Denmark -wanaoendeleza mashambulio ya angani.

Katibu mkuu wa Nato, Anders Fogh Rasmussen,

amewaambia mawaziri wa mambo ya nje mjini Berlin kuwa hajapata ahadi yoyote ya kuongezwa kwa ndege za kivita kutoka kwa washirika lakini ana matumaini kuwa hilo litafanyika.









Besigye wa Uganda apigwa risasi mkono








Besigye amekuwa akitembea kwenda kazini kama njia moja ya kufanya maandamano
Habari kutoka nchini Uganda zinasema kwamba kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye amepigwa risasi ya mkono na maafisa wa polisi ambao walikuwa wakijaribu kuwatawanya watu waliokuwa wakiandamana na kiongozi huyo wa upinzani mjini Kampala.

Awali polisi walijaribu kumzuia Besigye kutembea kwa miguu hadi kazini kama sehemu ya maandamano ya kupinga ongezeko la gharama ya maisha, lakini juhudi zao ziligonga mwamba baada ya raia kumzingira Besigye.

Watu kadhaa wakiwemo wabunge wawili wamekamatwa na polisi.

Kumekuwa na taarifa pia za maafisa wa polisi kutumia gesi ya kutoa machozi katika hospitali moja, baada ya waandamanaji kuanza kuwapura kwa mawe, walipokuwa wakiandamana na kulalamika juu ya ongezeko kubwa la bei za bidhaa muhimu na mafuta.

Mfanyakazi mmoja wa hospitali hiyo katika mji wa Kasangati, nje kidogo ya mji mkuu wa Kampala, amesema baadhi ya kina mama waliokuwa na watoto wagonjwa katika hospitali hiyo iliwabidi kuwahamisha watoto ili wasiathiriwe kwa gesi hiyo ya kutoa machozi.

Besigye kwanza alikamatwa siku ya Jumatatu, akiwa pamoja na wabunge wachache, waliokuwa wakishiriki katika maandamano kama ya leo.

Siku ya Alhamisi alikamatwa tena baada ya maandamano.

Mkuu wa polisi, Kale Kayihura, amesema maandamano hayo sio halali, na yeyote atakayeshiriki katika maandamano hayo atakamatwa.











Ben Ali wa Tunisa ashtakiwa




Serikali ya Tunisia imesema inataka kumshtaki aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Zine al-Abidine kwa makosa 18, ikiwemo kuua kwa kukusudia na magendo ya dawa za kulevya.

Waziri wa sheria Lazhar Karoui Chebbi amesema mashtaka hayo ni miongoni mwa 44 yaliyotolewa dhidi ya Bw Ben Ali, familia yake na baadhi ya waliokuwa mawaziri.

Hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Ben Ali inaandaliwa.




Alitolewa mwezi Januari wakati wa maandamano yaliyosababisha hata akakimbia nchi hiyo na kuelekea Saudi Arabia.

Serikali ilisema kwa wakati huo ilikamata wanafamilia 33, wakiripotiwa kushutumiwa kwa kupora mali ya nchi hiyo.

Katika mahojiano ya televisheni ya taifa siku ya Jumatano, Bw Chebbi alisema mashtaka 18 yametayarishwa dhidi ya Bw Ben Ali, ikiwemo "njama ya kulifisidi taifa, kuua kwa kukusudia na kufanya magendo ya dawa za kulevya." liliripoti shirika la habari la taifa la Tap













NATO yatathmini juhudi zake Libya





Mawaziri wa mashauri ya nje wa mataifa wanachama wa NATO wakutana Ujerumani kujadili juhudi zao Libya
Mawaziri wa mambo ya nchi za nje, na ambao ni wanachama wa muungano wa NATO, wanakutana mjini Berlin, Ujerumani, baada ya kuongezeka kwa ishara kuwa juhudi zao za kijeshi nchini Libya zimegonga mwamba.

Wanajeshi wa muungano huo walioko nchini Libya wameshindwa kuwasaidia wanajeshi wa waasi kumuondoa madarakani kiongozi wa taifa hilo Kanali Muammar Gaddafi.

Hapo jana waziri wa masuala ya nchi za kigeni wa Uingereza William Hague, alikiri kuwepo kwa mzozo wa kijeshi nchini Libya.

Uingereza na Ufaransa inazitaka nchi wanachama wengine wa muungano wa NATO kufanya juhudi zaidi ili kusaidia katika harakati za kuwashambulia wanajeshi wa Kanali Gadaffi










Obama ahimiza kubana matumizi




Rais Barack Obama ametoa pendekezo la kuongeza kodi kwa matajiri pamoja na kupunguza matumizi ya serikali kwa kile alichokiita mtazamo wa sawa katika kupunguza nakisi kubwa kwenye bajeti ya Marekani.

Katika hotuba mjini Washington DC alieleza mipango yake ya kuongeza kodi na kubana matumizi kwa nia ya kupunguza nakisi kwa dola trilioni $4 kufikia mwaka 2023.

Aliteta juu ya mipango ya chama cha Republican akisema mipango hiyo itaumiza masikini na watu wazee.

Wanachama wa Republican wamesema kuongezwa kwa kodi "si sawa".

"Lazima tuishi kulingana na uwezo wetu,kupunguza nakisi ya bajeti yetu,na tuanze mchakato utakaotuwezesha kulipa deni letu,"Bwana Obama alisema katika hotuba yake akiwa katika Chuo kikuu cha George Washington.

"Na lazima tufanye katika njia ambayo italinda uchumi wetu,na italinda wawekezaji,tunahitaji kukuwa, tuwe na nafasi za ajira,na tuwe na mustakabali mzuri."

Kuongezeka kwa nakisi kubwa katika bajeti ya Marekani kunatarajiwa kuwa suala kuu wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2012,na katika siku za hivi karibuni,wanachama wa Republican wameandaa mipango yao wenyewe ya kupunguza nakisi hiyo, ikiwa ni kupunguza matumizi ya bima ya afya na masuala mengine ya kijamii kwa watu maskini na wazee pamoja na matumizi katika elimu.

Nakisi hiyo ya bajeti inakisiwa itafikia dola trilioni $1.5 mwaka huu na wote wanachama wa chama cha Democratic na Republican wamesema kubana matumizi ni jambo la kupewa kipau mbele.










Muungano wa nchi zinazoijadili Libya



Muungano mpya wa nchi za kimataifa zinazompinga Kanali Muammar Gaddafi zimetoa wito wa kutaka kiongozi huyo aachie madaraka.

Umesema kuendelea kuwepo kwake kunatishia makubaliano yeyote yanayotarajiwa kufikiwa juu ya mgogoro nchini humo, na Walibya waruhusiwe kuamua wanayoyataka siku za usoni.

Wito huo umetolewa katika kauli ya mwisho iliyosomwa na mrithi wa kiti cha kifalme cha Qatar katika mkutano unaohusu Libya huko Doha.

Waasi wanaojaribu kumpindua Kanali Gaddafi wameshiriki kwa mara ya kwanza katika mkutano huo wenye hadhi ya juu wa kidiplomasia.

Muungano huo pia ulikubali kuendelea kuwapa waasi "vifaa"- maneno yanaoelezwa na mwandishi wa BBC Jon Leyne kuwa na utata-na pia wanafikiria kuwafadhili.

Awali, wajumbe waliambiwa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kuwa zaidi ya nusu ya jumla ya watu wa Libya ambao ni milioni sita huenda wakahitaji kupata msaada.

"Muungano" huo uliundwa katika mkutano wa kimataifa wa mawaziri mjini London Machi 29 yakiwemo mataifa ya Ulaya, Marekani, washirika wa Mashariki ya kati na mashirika mengine ya kimataifa








Allies pin hopes on Gaddafi’s swift exit







By James Blitz


The US, Britain and France want Muammer Gaddafi to pack up his bags in Tripoli and get out of the country.




Ten days after they began military action against the Libyan regime, this is the overwhelming goal of their strategy. The trouble is, however, that they need his departure to occur quickly if the coalition’s momentum is not to start flagging.




Over the past few days there has been much discussion about what the coalition’s goals are in Libya.

All three countries have made it clear, as they did at a conference in London on Tuesday, that they want a “new beginning” for the north African country.

All three have also been clear that getting rid of Colonel Gaddafi by direct military action is not their aim either. As President Barack Obama spelt out on Monday, regime change in Iraq “took eight years, thousands of American and Iraqi lives, and nearly a trillion dollars. That is not something we can afford to repeat in Libya”.

But the coalition leaders also know that there can be no better future for Libya – and no closure to their own military engagement – unless Col Gaddafi departs the scene. As a result, they are now piling the military, political and psychological pressure on him to do so.


Thus far they have reasons to be hopeful. The international operation against the Libyan leader has gone well.




The opposition rebels have made strides in recent days, helped by western air strikes on Gaddafi installations, and are in control of a vast portion of the country’s oil wealth. The coalition air strikes have taken place without signs of civilian casualties.

One other factor also gives comfort to the allies: the repeated mistakes that Col Gaddafi has made in this conflict. Repeatedly he has called ceasefires, only to break them, under-mining his credibility.



He has left his tanks and armoured vehicles out in the open, allowing more of them to be destroyed than the coalition had expected. The international media coverage of Eman al-Obeidi, the woman who was seized by Gaddafi henchmen while claiming she had been raped by his loyalists, is a particularly striking own goal.

“Gaddafi has always been cunning in the way he brutalises his opponents,” says a British official. “But when it comes to strategy, you could hardly call him clever.”

The hope in western capitals is that all of these developments might presage a collapse of support for Col Gaddafi in Tripoli. But the risk is that, if he digs in, it will be harder to maintain coalition momentum.

Two issues are of particular concern. First, there are limits to how far the coalition – which on Wednesday moves to Nato command – can degrade Col Gaddafi’s capability. UN Security Council resolution 1973

mandates the coalition to protect civilians. But the coalition’s military action is going beyond this.

On Monday, it bombed regime installations in Sirte, Col Gaddafi’s birthplace,


where there has been scarcely any rebellion. It will be hard to keep up such actions if they are merely providing cover for a rebel advance.

The second concern is over the actions of the rebels. In the early stages of the conflict they could be cast as victims of repression. But as they gain momentum, the international media is taking an increasingly hard look at them.

There is lingering uncertainty about who the rebels are and what they represent. No less worrying are their tactics.

On Monday there were reports that the rebels had fired rockets and missiles into Sirte


for a few hours, without any idea whether they were hitting Gaddafi forces or civilians. If the west’s avowed mission is to protect the local population, actions such as this may prove to be a problem.

Inside the western coalition, senior figures insist they still have the upper hand. “I don’t think we need to be bound by a hard deadline as to when we need Gaddafi to be out,”

says one western diplomat. “The important thing is to keep up the momentum against him and not let it drop away.”


But there are those who argue that success needs to come quickly. Put simply, if Col Gaddafi is still in Tripoli in two or three weeks’ time, western leaders will start worrying.








Ouattara aahidi kuleta haki Ivory Coast





Rais mpya wa Ivory Coast Alassane Ouattara amesema pande zote zilizohusika katika ghasia lazima zishtakiwe.

Alisema ataiomba mahakama ya kimataifa ya uhalifu kufanya uchunguzi juu ya mauaji ambapo majeshi yake na ya mpinzani wake Laurent Gbagbo yanahisiwa kuhusika.


Bw Alassane Ouattara




Bw Gbagbo alikamatwa siku ya Jumatatu na majeshi ya Bw Ouattara baada ya kukataa kuwa alishindwa kwenye uchaguzi wa mwezi Novemba.


Bw Ouattara alisema, sasa atakabiliwa na mashtaka "katika kiwango cha kitaifa na cha kimataifa."

Katika mkutano uliofanyika kwenye mji wa kibiashara wa Abidjan, Bw Ouattara alisema Bw Gbagbo amepelekwa eneo salama.

No comments:

Post a Comment