Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Friday, April 22, 2011

Ijumaa Kuu



Ijumaa Kuu ni siku ya mwaka ambayo wafuasi wengi wa Yesu Kristo wanaadhimisha kifo chake msalabani ambacho kilitokea nje ya kuta za mji wa Yerusalemu siku ya Ijumaa.


Kadiri ya Mtume Yohane kesho yake ilikuwa Sabato na pia Pasaka, jambo lisilotokea kwa kawaida. Kwa sababu hiyo wataalamu mbalimbali wanakadiria ilikuwa tarehe 7 Aprili 30.

Ijumaa kuu ni sehemu ya Juma Kuu linaloanza kwa adhimisho la Yesu kuingia mji huo akishangiliwa kama mfalme wa Wayahudi (yaani Masiya au Kristo). Adhimisho hilo linafanyika mwanzoni mwa wiki, yaani Jumapili ya matawi.

Ijumaa kuu ni pia sehemu ya siku tatu kuu za Pasaka zinazoadhimisha mateso na kifo chake, kulala kaburini, na hatimaye kufufuka kwa utukufu




Yesu




Yesu alikuwa Myahudi mwanamume aliyeishi miaka 2000 hivi iliyopita (labda 6 KK - 30 B.K.). Kutokana na umuhimu wake katika historia ya binadamu, kwa kawaida miaka yote inahesabiwa kwanzia ujio wake (ulivyokadiriwa kimakosa katika karne ya 6).



Mazingira yake




Nchi ambayo Yesu alizaliwa akafundisha ni nchi ileile ambayo Mungu aliwaahidia Waisraeli tangu zamani za Abrahamu, ni nchi ileile waliyoiteka chini ya Yoshua, ni nchi ileile waliyoirudia kutoka utumwani Babeli.


Lakini wakati wote wa Agano Jipya, yaani tangu Yesu alipozaliwa hadi mwisho wa maisha ya mitume wake, nchi hiyo haikuwa huru, bali chini ya himaya ya Warumi, ingawa pengine hao waliwakabidhi vibaraka, yaani watawala wenyeji waliowekwa na wakoloni.

Vibaraka hao ni Herode Mkuu (37 KK-4 KK) na wazawa wake, ambao tena hawakuwa Waisraeli halisi bali Waedomu ingawa kabila lao lililazimishwa kuingia dini ya Kiyahudi karne iliyotangulia. Ukoo huo unajulikana kwa ukatili, uchu wa madaraka na uzinifu wake.

Vilevile maliwali wa Kirumi waliowekwa pengine kutawala nchi au sehemu fulani walionyesha mara nyingi ukatili na dharau kwa Waisraeli na dini yao, hata kusababisha chuki na mapigano kati ya jeshi na wananchi. Mfano mmojawapo ni Ponsyo Pilato aliyesimamia Uyahudi kuanzia mwaka 26 hadi 36 B.K.

Mbali na hayo, utawala wa Roma, ulioenea Ulaya Magharibi na Kusini, Afrika Kaskazini na nchi za Mashariki ya Kati kupakana na Iraq ya leo, kwa jumla ulihakikisha hali ya amani kwa muda wote wa Agano Jipya na karne za kwanza za Kanisa. Hali hiyo, pamoja na umoja wa dola hilo lote, na urahisi wa mawasiliano kwa njia ya barabara zilizotengenezwa na Warumi, na uenezi wa lugha ya kimataifa (Kiyunani yaani Kigiriki cha zamani), ilichangia kasi ya uenezaji wa habari njema (Injili). Lugha hiyo ndiyo iliyotumiwa na waandishi wote wa Agano Jipya ili vitabu vyao viwafaidishe watu wengi zaidi, ingawa baadhi yao hawakuijua vizuri.

Lugha asili ya Yesu na ya Mitume ilikuwa Kiaramu ambacho ni jamii ya Kiyahudi na ambacho polepole kilishika nafasi yake kati ya Wayahudi kuanzia karne ya sita K.K. Hao wote walitokea mkoa wa Galilaya, uliokuwa na mchanganyiko wa watu (Waisraeli na mataifa), kiasi kwamba huko Wayahudi wenyewe walifuata kwa urahisi desturi za Kiyunani hata wakadharauliwa na wenzao wa Kusini (Yerusalemu na mkoa wa Yudea).

Kati ya mikoa hiyo miwili ulienea mkoa wa Samaria ambao wakazi wake walijenga uadui mkubwa na Wayahudi baada ya uhamisho wa Babeli, walipokataliwa kuchangia ujenzi wa hekalu la pili la Yerusalemu.






Maisha yake


Dionisi Mdogo, mmonaki aliyeanzisha (mwaka 533 hivi) mtindo wa kuhesabu miaka kuanzia kuzaliwa Yesu kurudi nyuma (K.K.) au kwenda mbele (B.K.), alikosea hesabu zake. Leo tunakisia Yesu alizaliwa mwaka 6 hivi K.K. kwa sababu alizaliwa Bethlehemu chini ya

Mkuu aliyefariki mwaka 4 K.K.

Huyo alipojaribu kumuua mtoto Yesu, familia takatifu ilikimbilia Misri mpaka baada ya kufa kwake. Hapo ikarudi Galilaya hata Yesu akajulikana kwa jina la kijiji cha Nazareti kilichodharauliwa na Wagalilaya pia. Ndipo alipokulia na kuishi akifanya kazi ya ufundi.

Mwaka 26 hivi B.K. ndugu yake Yohane Mbatizaji aliacha maisha ya jangwani na kuanza kuhubiri toba kandokando ya mto Yordani. Kwa kuwa Waisraeli walikosa manabii kwa muda mrefu, na walitamani sana ukombozi, walimuendea kwa wingi hata wakamtia hofu Herode Antipa.

Ingawa huyo akamfunga mapema akamuua, kazi ya Yohane ilikuwa imetimia kwa sababu aliweza kuwaandaa Waisraeli wengi (hasa watu wadogo na wakosefu) wampokee Yesu aliyebatizwa naye. Katika nafasi hiyo Yohane alimtambulisha kama Mwanakondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu.

Ndipo Yesu naye alipoanza kuhubiri, lakini pia kutenda miujiza ya kila aina, akapata haraka wafuasi wengi. Kati yao akachagua Mitume wake 12 kama msingi mpya wa taifa la Mungu. Alifanya kazi hizo kuanzia Galilaya, akitangaza ujio wa ufalme wa Mungu, kwa maana ya kwamba ufalme uliotazamiwa na Wayahudi umewajia kwa njia yake.

Ingawa hakupitia shule yoyote ya Biblia, Yesu alionekana anafundisha vizuri kuliko walimu wa sheria wa kawaida, kama mtu mwenye mamlaka juu ya Torati. Mafundisho yake yalilingana na yale ya Mafarisayo kuliko na yale ya Masadukayo, lakini alishindana pia na hao wa kwanza.

Kijicho na upinzani vikazidi hasa Yerusalemu, walipoanza kufanya njama za kumuua. Ingawa Yesu alijua hayo, alijikaza kwenda katika mji mtakatifu autangazie habari njema na kufia huko. Baada ya kupokewa kwa shangwe kabla ya sherehe ya Pasaka ya mwaka 30 (au 33) akakamatwa na baraza la Israeli kwa tuhuma ya kufuru ya kujilinganisha na Mungu, halafu akakabidhiwa kwa liwali wa Kirumi aliyekuwa na mamlaka ya kutoa adhabu ya kifo. Baada ya kikao ambapo Wayahudi walitafuta kisingizio cha kisiasa, Ponsyo Pilato akalazimika kuagiza Yesu asulubiwe, na kisha kufa kwake kaburi lilindwe na askari.

Hata hivyo siku ya tatu kaburi likaonekana tupu, na Yesu akaanza kuwatokea wanafunzi wake wa kike na wa kiume kwa muda wa siku arubaini, halafu akapaa mbinguni mbele ya macho yao.

Habari hizo zikatangazwa kwa sauti tu kwa miaka kadhaa, halafu zikaanza kuandikwa. Kanisa linaheshimu kwa namna ya pekee, kama ushuhuda mkuu juu ya maisha na mafundisho ya Yesu na kama moyo wa Maandiko matakatifu yote, Injili nne zilizoandikwa na Marko, Mathayo, Mwinjili Luka na Yohane kati ya mwaka 65 na 100 hivi.






Imani juu yake





Waumini wake wanaunda Kanisa la Kikristo ambalo linapatikana leo katika madhehebu mengi.


Karibu wote wanamwamini kuwa Mungu aliyechukua umbile la mwanadamu au, kwa lugha nyingine, kuwa Mwana wa Mungu. Wakristo wengine wanaamini kuwa yeye ni mtume wa pekee wa Mungu ila sio Mungu.


Katika dini ya Uislamu, Yesu anajulikana kama Nabii Isa. Waislamu wanaamini kuwa yeye alikuwa ni nabii wa Mungu ila hakuwa mwana wa Mungu wala Mungu. Vile vile waislamu hawaamini picha au Sanamu ya mtu ambae wakiristo wanamwita yesu.
Waislamu wanaamini kwamba hakuna picha hata moja ya mitume wa Mungu iliopatikana wala iliopo duniani. Wanadai kama ingelikuwepo picha ya mtume yeyote, basi watu wangevuka mpaka na kuanza kuabudu picha hiyo na kumsahau Mungu wao au wakachanyanya imani ya picha, mhusika pamoja na Mungu, kitu ambacho katika uislamu ni kumshirikisha Mungu na viumbe wake.

Waislamu wanaamini kwamba yesu alizaliwa kutokana na nguvu ya Mungu. Waislamu wanaamini kwamba yesu kuzaliwa bila ya Baba ni sawa na Adamu na Hawa kuwepo duniani bila BABA WALA MAMA. ADAMU na Hawa ndio binadamu wenye ukosefu wa BABA,MAMA wala walikuwa hawana ndugu,jamaa na marafiki katika maisha yao. bali wao Mungu aliwafanya kuwa chanzo chetu sisi binadamu.

Waislamu hawaamini kwamba yesu alikufa wala aliuliwa na wayahudi wenzake, bali waislamu wanaamini kwamba yesu aliondolewa katika Mateso ya Wayahudi, na yuko mbinguni upande wa kulia wa Mungu. Waislamu wanamini kwamba kuna siku yesu atarudi duniani na kutatuwa matatizo yalioko baina yao na dini nyingine.






Maadhimisho yakeMaisha yake yamekuwa msingi wa sikukuu mbalimbali




zinazosheherekewa katika nchi nyingi duniani, kama vile Noeli au Krismasi (kuzaliwa kwake), Epifania (kuonekana kwake na kubatizwa kwake), Majilio (kuandaliwa ujio wake), Kwaresima (mafungo na mateso yake), Ijumaa Kuu (kifo chake); muhimu kuliko zote ni Pasaka (kufufuka kwake).







Misingi ya ujuzi wetu juu yake


Papyrus P52, iliyoandikwa kwa Kigiriki mwaka 125 hivi, inahesabika kuwa andiko la zamani zaidi kutufikia kuhusu Yesu. Ina sehemu za Injili ya Yohane; mbele 18:31-33, nyuma 18;37-38


Yesu hakuacha maandiko yoyote. Habari zake zinapatikana hasa katika Biblia, kwa namna ya pekee katika Injili.

Nje ya Ukristo kuna habari fupi kuhusu Yesu katika maandiko ya waandishi Waroma, Wagiriki na Wayahudi. Habari hizi zinaangaliwa sana kwa sababu zimetungwa na watu wasiomwamini Yesu. Kwa ujumla zinathibitisha ya kwamba Yesu alikuwepo, alikuwa na wafuasi huko Roma na ya kwamba awali Waroma hawakuelewa tofauti kati ya wafuasi wake na Wayahudi. Muhimu ni hasa:

1. Mtaalamu Myahudi Flavius Josephus aliandika mnamo 90 B.K. kitabu cha „Antiquitates Judaicae“ (Habari za historia ya Kiyahudi) akitaja kifo cha „Yakobo ndugu wa Yesu“ (sura ya 20, 200).

2. Mwandishi Mroma Tacitus aliandika mnamo mwaka 117 ya kwamba Kaisari Nero alishtaki kikundi cha “Chrestiani” ya kuwa wamechoma moto mji wa Roma. Aliongeza: “Mtu ambaye ni asili ya jina hili ni Chrestus aliyeuawa wakati wa Tiberio kwa amri ya Pontio Pilato” (Annales XV,44).

3. Mwandishi Mroma Svetonius alimtaja “Chrestos” katika kitabu chake juu ya maisha ya Kaisari Claudius (25,4) ya kwamba huyu amesababisha fujo kati ya Wayahudi wa Roma hivyo Kaisari aliwafukuza mjini.

4. Mwanasiasa Mroma Gaius Plinius Caecilius Secundus aliacha barua kadhaa zinazotaja Wakristo mnamo mwaka 100 B.K. Alimwuliza Kaisari Traianus jinsi ya kushughulikia Wakristo waliokataa kutoa sadaka mbele ya sanamu za Kaisari.













Marekani kufanya mashambulizi Libya






Robert Gates
Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Robert Gates amesema ndege za kivita zisizokuwa na rubani zinatekeleza mashambulizi ya anga nchini Libya.

Gates amesema utumizi wa ndege hizo uliidhinishwa na rais Obama na kwamba zitaongeza uwezo wa wanajeshi wa muungano wa NATO katika harakati zao za kijeshi nchini humo.







Waasi nchini Libya, wamekuwa wakipambana na wanajeshi wa Kanali Gadaffi tangu mwezi Februri mwaka huu, lakini wameanza kupiga hatua ndogo.


Katika kikao na waandishi wa habari mjini Washington, Gates amesema kwamba rais Obama aliidhinisha utumizi wa ndege hizo maalum zisizo na rubani kama mchango wao na pia kudhihirisha uwezo wao wa kijeshi.



Ndege za kivita za Marekani
Amesema ndege mbili zitakua chini ya usimamizi wa NATO kwa saa 24 kila siku.

Bwana Gates, amekanusha madai kuwa kutumwa kwa ndege hizo ni ishara ya Marekani ya kujiunga na Muungano wa NATO katika harakati zake za kijeshi nchini Libya, kwa njia ya siri.



Ndege hizo maalum za kurusha makombora zinatumika kuwalenga wapiganaji wa waasi katika mipaka ya Pakistan na Afghanistan.

Idara ya ulinzi ya Marekani imesema ndege hizo zitakuwa na uwezo wa kuwatambua wanajeshi wa Gadaffi ikiwa watajificha ndani ya magari ya kibinafsi au wakiingia kwenye maeneo ya makaazi ya watu.

Ndege hizo zina uwezo wa kupaa muinuko wa chini kuliko ndege zingine za kivita na hivyo kuifanya bora katika juhudi za kijasusi na kufanya mashambulio, kwa kuwa ni vigumu kwa ndege hizo kuonekana kwenye mtambo wa rada.

Wataalamu wanasema hii ni ishara tosha kuwa Marekani inajihusisha zaidi katika mzozo huo nchini Libya.














Biden, Putin discuss trade, missile defense








by Staff Writers

Washington (AFP) April 21, 2011
US Vice President Joe Biden and Russian Prime Minister Vladimir Putin on Thursday discussed Moscow's goal of joining the World Trade Organization and missile defense cooperation, the White House said.
Biden and Putin talked about "the Obama administration's commitment to terminate" the application to Russia of a Cold War-era US law that blocks certain non-market economies that restrict emigration from joining the WTO.

They also discussed "next steps on missile defense cooperation" and "agreed on the importance of continuing momentum in relations between the United States and Russia," according to a White House statement.

"Vice President Biden underscored the continued need for cooperation between the United States and Russia on global security issues and pledged to continue to work with Russia on facilitating travel between our two countries," it said.

Moscow needs Washington to stop applying the so-called Jackson-Vanik law to Russia in order to gain US "permanent normal trade relations" -- and be cleared for WTO accession.

Russia is the last major economic power to lack WTO membership.

The conversation came a day after Putin needled the United States over its deficits and national debt and accused Washington of "behaving like a hooligan" by flooding world markets with devalued dollars.

"Look at their trade balance, look at the budget deficit, at the debt of the United States," Putin said in closing comments to his annual address to parliament.

"We have none of that -- and, I hope, we never will," Putin said to a strong round of applause.

No comments:

Post a Comment