Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Wednesday, August 4, 2010

Ngono ya Bure Iwapo Uholanzi Itatwaa Kombe la Dunia

Kombe la dunia halikosi vituko, msanii mwanamke wa filamu za ngono raia wa Uholanzi, ametoa ahadi ya kuwanyonya watu sehemu zao za siri iwapo Uholanzi itatwaa kombe la dunia.
Msanii wa filamu za ngono Bobbi Eden ametoa ahadi ambayo haijawahi kutokea kama zawadi ya ubingwa wa kombe la dunia.

Kwa mujibu wa gazeti la Huffington Post la Marekani, Bobbi Eden amewaahidi wafuasi wake wote kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa iwapo Uholanzi itaifunga Hispania kwenye mechi ya fainali ya kombe la dunia basi atawanyonya wafuasi wake wote wa kiume sehemu zao za siri.

Bobbi sio mwanamke wa kwanza kuahidi masuala ya ngono kama zawadi ya ubingwa wa kombe la dunia mwaka huu.

Mrembo mwanamitindo wa Paraguay, Larissa Riquelme aliahidi kukimbia uchi kwenye mitaa ya Paraguay iwapo timu hiyo ingetwaa kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Kwakuwa Paraguay ilitolewa mapema kwenye fainali hizo, Larissa asingelazimika kutimiza ahadi yake lakini ameahidi kukimbia uchi kama zawadi kwa wachezaji wa Paraguay.

Wakati huo huo, Diego Maradona naye aliahidi kukimbia bila nguo kwenye mitaa ya katikati ya jiji la Buenos Aires iwapo Argentina ingetwaa kombe la dunia.

Mradona alisema hivyo wakati alipohojiwa na radio moja nchini humo baada ya Argentina kuifunga Kanada 5-0 wakati wa mechi ya mwisho ya kujiandaa na kombe la dunia.

"Kama tukishinda kombe la dunia, nitavua nguo zote na kukimbia katikati ya mji", alisema Maradona.

Hata hivyo Argentina ilitolewa na Ujerumani kwenye robo fainali kwa kubugizwa mabao 4-0.

No comments:

Post a Comment