Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Tuesday, February 1, 2011

Usingizi relini

Bwana mmoja nchini Japan, baada ya kutoka katika matembezi yake ya usiku ambapo alikuwa amekunywa pombe kikamilifu, alipitiwa na usingizi wakati akirejea nyumbani na kulala juu ya reli.


Reli



Bwana huyo kutoka Chiba Prefecture , mapema wiki hii aliuchapa usingizi kisawasawa katikati ya mataruma ya reli na kuanza kukoroma.

Dereva wa treni ya mizigo iliyokuwa ikipita katika reli hiyo, aliweza kumuona bwana huyo , na mara moja akaweka breki za dharura kuisimamisha treni hiyo iliyokuwa katika mwendo wa kasi.


Kwa bahati mbaya, au nzuri, treni hiyo ilishindwa kabisa kusimama, na kupita juu ya mlevi huyo, ambaye aliendelea kukoroma bila kujua kinachotokea. Baadaye mlevi huyo alishituka, na kukuta behewa la treni limesimama juu yake, na hivyo kulazimika kutambaa na kutoka chini ya treni hiyo.

Mtandao wa habari wa Japanator umesema wachunguzi wanasema, bwana huyo ana bahati kubwa kwani kulikuwa na nafasi ya kutoka kati ya trenni ya reli, la sivyo angesagwasagwa. Tukio hilo lilisababisha kuchelewa kwa treni tatu kwa karibu dakika kumi na nne, na kusababisha usumbufu kwa abiria wapatao mia saba.

No comments:

Post a Comment