Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Tuesday, February 1, 2011

Party za Krismasi


Krismasi



Wafanyakazi wengi wanadhani sherehe za kiofisi za Krismasi zitaharibiwa iwapo wakuu wa kazi nao watahudhuria sherehe hizo.


Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa, mbali na wafanyakazi kona kwamba hawataweza kufanya vituko vyao, pia wanakuwa na mashaka ya nguo watakazovaa, ambazo huenda mabosi wao wakawa waharidhiki nazo sana. Utafiti huo umefanywa na mgahawa wa TGIF. Katika watu elfu mbili waliohojiwa, asilimia 27 walisema wana wasiwasi huenda wakashindwa kujizuia kusema jambo ambalo halitamfurahisha mkuu wake wa kazi -- hasa baada ya kuwa wamepata kinywaji.


Wengine hata wamehisi kuwa huenda wakazusha ugomvi wa kurushiana makonde. Robo ya watu hao wamesema kuwepo kwa bosi wao kunapunguza watu kuwa na raha, wakati mmoja kati ya watu watano wamesema ni bora mabosi hao wasihudhurie kabisa sherehe hizo.

Asilimia moja ya watu hao wamesema walilazimika kuacha kazi baada ya party hizo za kiofisi za mwisho wa mwaka. Mkurugenzi wa mauzo wa TGIF Darrel wade amesema "sherehe za kiofisi za Krismasi ni watu kufurahia na kusherekea kwa kazi walizofanywa kwa mwaka mzima.-- Mabosi wanaotaka kwenda katika sherehe hizo, wanatakiwa wawaachie huru wafanyakazi wao."

No comments:

Post a Comment