Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Saturday, November 27, 2010

Mwanaume Abakwa na Wanawake 10


Kijana mwenye umri wa miaka 17 wa nchini Papua New Guinea amelazwa hospitali akipatiwa matibabu baada ya kubakwa genge la wahuni wanawake wapatao 10.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa Southern Highland, nchini Papua New Guinea, Teddy Tei, kijana huyo mwenye umri wa miaka 17 alikumbana na zahama hilo siku ya ijumaa wakati alipovamiwa na kundi la wahuni wanawake wapatao 10.

Wanawake hao wakiwa na visu walimshambulia kijana huyo kabla ya kupokezana kumbaka kwa zamu.

"Hii ni kesi tunayoifualia kwa ukaribu zaidi, tunawatafuta wanawake waliofanya unyama huu", alisema kamanda huyo wa polisi.

Taarifa ya polisi ilisema kwamba wanawake 10 wakiwa na visu walimshambulia kijana huyo na wanawake wanne kati yao walimuingilia kinguvu kijana huyo.

Kamanda Tei aliongeza kuwa kijana huyo aliwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi.

Kijana huyo ambaye jina lake limewekwa kapuni, anafanyiwa uchunguzi ili kujua kama ameambukizwa magonjwa ya zinaa au la.

"Ugonjwa wa ukimwi ni tatizo kubwa hapa Papua New Guinea, ninahofia huenda baadhi ya wanawake waliombaka huenda wakawa ni waathirika", alisema Kamanda Tei na kuongeza.

"Nimekuwa nikiwaonya wanawake wawe waangalifu sasa inanibidi nianze kuwaonya na wanaume nao wawe waangalifu mitaani".

No comments:

Post a Comment