Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Friday, June 10, 2011

Malawi yazuwia ruzuku za wagonjwa wa HIV

Serikali ya Malawi imesimamisha kutoa ruzuku maalum kwa watumishi wa serikali wenye virusi vya HIV na UKIMWI kwa sababu inasema wanatumia fedha hizo kwa kunywa pombe na kuwapa makahaba.

Serikali ya Malawi imesimamisha kutoa ruzuku maalum kwa watumishi wa serikali wenye virusi vya HIV na UKIMWI kwa sababu inasema wanatumia fedha hizo kwa kunywa pombe na kuwapa makahaba.


mchango kwa wagonjwa wafujwa

Takriban watumishi wa serikali elfu 40 wamenufaika na mpango huo.

Serikali ya Malawi inawashtumu watumishi wa serikali nchini humo kwa kueneza zaidi virusi vya HIV na UKIMWI Kwa kutumia fedha hizo kujihusisha na vitendo vinavyohatarisha maisha.



Makahaba hupokea fedha za msaada

Kuanzia sasa kila mwezi watapokea posho ya chakula cha lishe bora badala ya kupokea fedha za ziada.

Afisa moja asema mpango huo umetumiliwa vibaya zaidi na watumishi wa serikali wanaojidai kua nao pia wamambukizwa na virusi vya HIV ili wajipatie fedha zaidi..Takriban asilimia 15 ya wakaazi wa Malawi wana virusi vya HIV,na idadi kubwa ya vifo kutokana na ugonjwa huo umepunguza kiwango cha maisha kufikia umri wa wastani wa miaka 36





Muafaka kuhusu serikali ya mpito Somalia





Wafuasi wa Waziri mkuu mjini Mogadishu

Waziri Mkuu Mohammed anatakiwa kujiuzulu chini ya siku 30

Viongozi wa Somalia wamekubaliana kusitisha uhasama wa kisiasa kati yao baada ya mzozo uliodumu miezi kadhaa.

Rais Sheikh Sharif Sheikh Ahmed na Spika wa Bunge Sheikh Sharif Aden wamekubaliana kuhairisha uchaguzi hadi mwezi Agosti mwaka ujao.

Utata huo wa viongozi umesababisha kuzorota kwa uhusiano kati ya serikali ya mpito na jumuiya ya kimataifa.

Jumuiya ya kimataifa ilikuwa inashinikiza uchaguzi ufanyike Agosti mwezi huu baada ya muhula wa serikali hii ya mpito kukamilika.

Viongozi hao wametia saini muafaka wa kusitsha usahama kati yao mjini Kampala Uganda kufuatia juhudi za upatanishi zilizoongozwa na mwenyeji wao Yoweri Museveni.

Kulingana na mkataba huo, Waziri Mkuu Mohammed Abdullahi Mohammed atatakiwa kujiuzulu chini ya siku thelathini baada ya kusainiwa mkataba huo. Rais Sharif atateuwa mtu mwengine kuchukua nafasi hiyo.

Hata hivyo hatua hiyo imepingwa vikali na wafuasi wa Waziri Mkuu Mohammed, ambao wamefanya maandamano makubwa mjini Mogadishu.

Waziri Mkuu Mohammed alikuwepo mjini Kampala lakini anasemekana kuwa amerudi nchini Somalia.

Kulingana na taarifa kutoka mwakilishi wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa nchini Somalia, Balozi Augustine Mahiga, viongozi wa Afrika Mashariki chini ya shirika la maendeleo la IGAD, watasimamia mkataba huo kuhakikisha unatekelezwa.

Nchi za kigeni zinazofadhili mikakati ya amani nchini Somalia, mara kadhaa zimeelezea kero zao kuhusu uhasama wa mara kwa mara wa kisiasa kati ya viongozi nchini humo.

Tofauti hizo za kisiasa ambazo wadadisi wa siasa za Somalia wanasema zinachochewa na uchu wa madaraka, zinasemekana kuchangia uzembe wa jumuiya ya kimataifa wa kuisaidia nchi hiyo kujikwamua kutoka vita vilivyo dumu miaka ishirini.







Afrika Mashariki yakabiliwa na Njaa








Shirika moja la kimarekani limeonya kuwa janga kuu la uhaba wa chakula duniani linaendelea kubana mashariki mwa upembe wa Afrika.
Njaa



Uhaba wa chakula waathiri Afrika Mashariki

Shirika hilo lijulikanalo kama The Famine Early Warning Systems Network limeonya kuwa nchi zinazotia wasiwasi ni Ethiopia, Kenya na Somalia.


Limesema usaidizi mkubwa wa dharura unahitajika kuokoa maisha na kukabiliana na utapiamlo katika eneo hilo.

Shirika hilo pia limesisitiza kuwa usaidizi unaotolewa kwa sasa hautoshi.

Katika taarifa yake shirika hilo limesema kuwa eneo la upembe wa afrika limeathiriwa na upungufu wa mvua kwa misimu miwili hivyo kusababisha ukame mbaya zaidi tangu mwaka 1995







Uturuki haitawakataa wakimbizi wa Syria





Ambulensi za Uturuki

Magari ya kubebea wagonjwa ya Uturuki yakiwasaida waliojeruhiwa Syria

Waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema nchi yake haitafunga mipaka yake kwa wakimbizi kutoka Syria, wakati mamia ya watu wamekuwa wakiitoroka nchi hiyo, kutokana na msukosuko wa kisiasa.

Bw Erdogan amesema anafuatia kwa makini matukio nchini Syria, na amemsihi rais Bashar al Assad kutekeleza mapendekezo ya mabadiliko ya kisiasa.

Mwandishi wa BBC aliye mpakani kati ya Uturuki na Syria ameelezea kwamba magari ya kubebea wagonjwa kutoka Uturuki yamekuwa yakivuka mpaka na kuingia Syria katika siku za hivi karibuni, na kurudi Uturuki yakiwa yamewabeba watu waliojeruhiwa katika maandamano ya kuipinga serikali ya Syria.

Ameelezea pia kuna raia wa Syria ambao wanaonelea badala ya kuvuka mpaka na kuingia Uturuki kama wakimbizi, ni afadhali kuishi katika hema hafifu walizojitengenezea, mita mia chache kutoka eneo la mpakani.








Rais Saleh wa Yemen 'aliumia' sana




Saleh

Rais wa Yemen Ali Abdallah Saleh anayedaiwa kujeruhiwa vibaya

Rais wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, alijeruhiwa zaidi katika shambulio la makombora katika boma lake juma lililopita kuliko ilivyodhaniwa, maafisa wa Serikali wameambia vyombo vya Habari vya Marekani.

Maafisa wa Serikali waliambia shirika la Habari la AP kuwa Bwana Saleh alichomeka asilimia 40 ya mwili wake na anavuja damu katika fuvu lake kutokana na shambulio hilo la Ijumaa.

Rais anaendelea kupata matibabu nchini Saudi Arabia baada ya kushambuliwa katika Ikulu yake katika Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa.

Afisa wa cheo cha juu Serikalini aliambia BBC kuwa hawatasema lolote kuhusiana na afya ya Rais Saleh.

"Sisi si madaktari. Na kama Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, Bi Hillary Clinton alivyosema jana, sisi tuko hapa na Sanaa na tunafanya kila juhudi kuhakikisha kuwa tunaleta mabadiliko kwa utaratibu, amani na bila ghasia, kama inavyosema Katiba ya Yemen," afisa huyo alisema.
Uwezo wa kutawala


Kaimu kiongozi, Makamu wa Rais Abd-Rabbu Mansour Hadi, alisema Bwana Saleh anatarajia kurejea baada ya siku chache.

Lakini wachunguzi wanasema kuwa kiwango cha majeraha ndicho kitakachoamua ni lini - na ikiwezekana - ikiwa atarudi katika taifa hili lenye umuhimu mkubwa ambalo amelitawala kwa zaidi ya miaka 33. Hali hiyo pia itaamua ni nani atakayechukua mamlaka iwapo yeye hatakuwa na uwezo wa kutawala.
Jaribio la kutaka Kuua

Haikujulikana kiwango cha alivyochomeka na kiwango cha majeraha alichokuwa nacho lakini Jumamosi wandani kadhaa wa Rais Saleh walisema kuwa alichomeka kwenye kifua na uso na kwamba mabaki ya kombora yalipenyeza chini ya moyo wake.

Rais alifanyiwa upasuaji Jumatatu ili kuondoa vipande vya mbao katika kifua chake na pia kumtibu majeraha ya moto kwenye uso na kifua, kama shirika la AP linavyoripoti.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 69 hajaonekana tangu Ijumaa wakati makombora yalipotumika kushambulia Ikulu ya Rais na kuwaua watu saba na kuwajeruhi maafisa kadhaa wa vyeo vya juu Serikalini katika tukio ambalo maafisa hao wa Serikali wanasema ni jaribio la kutaka kuwaua.








Marekani yataka Gaddafi ang'olewe haraka








Marekani imeyaomba mataifa ya Magharibi na ya Kiarabu kuongeza juhudi katika azma ya kumng'oa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi.

Waziri wa mashauriano ya nchi za kigeni Bi Hillary Clinton amesema huu ndio wakati wa kumtimua Gaddafi.




Bi Clinton akihutubia mkutano wa Abu Dhabi

"Huu ni wakati wetu,mazingira yanaturuhusu.Gaddafi amefika kikomo'', Bi Clinton alisema katika mkutano wa viongozi wanaokutana mjini Abu Dhabi.



Bi Clinton pia aliwaambia wajumbe kuwa lazima juhudi zaidi zifanywe za kumbana Gaddafi na utawala wake kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi.

Mkutano huo wa Abu Dhabi unatarajiwa kukamilisha mipango ya kuanzisha hazina maalum ya kuwasaidia waasi wa Libya.



Waakilishi wa nchi za Uingereza, Ufaransa, Marekani, Jordan, Kuwait na Qatar wanakutana ili kupanga jinsi Libya itakavyokuwa baada ya kumtimua Gaddafi uongozini.


Wakati huo huo Tripoli imekanusha madai ya uhalifu wa kivita ambayo yamewasilishwa mbele ya baraza la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binaadamu mjini Geneva.

Baraza hilo la Umoja wa Mataifa kwa wakati huu linajadili madai ya ukiukaji wa haki za binaadamu yanayodaiwa kutekelezwa na upande wa serikali pamoja na waasi.


Lakini mwanadiplomasia wa Libya Mustafa Shaban ameliambia baraza hilo kuwa upande wa serikali hauna hatia yeyote kwani ndio unaoshambuliwa.Na amelaumu vyombo vya habari, upinzani na mamluki wa kigeni kwa kukiuka haki za kibinadamu nchini Libya ikiwemo ukatili dhidi ya watu.










PRESIDENT OBAMA SUPPORTS WORLD FUTURE ENERGY SUMMIT HELD IN ABU DHABI





Abu Dhabi, 12 January 2011: In a guide to U.S. exhibitors attending the World Future Energy Summit, the President of the United States of America, Barack Obama, acknowledged the role of Abu Dhabi’s WFES in increasing economic growth and creating jobs. The letter follows on from Secretary of State Hillary Clinton’s visit to Masdar on Monday.

“Selected by the U.S. Department of Commerce as part of the U.S. Commercial Service’s Trade Fair Certification Program, this prominent trade exhibition is an excellent venue for developing new business,” wrote President Obama. “By opening new markets and promoting trade, we are creating new sales channels for U.S. products and services. The business relationships developed at this trade show will help increase economic growth and create jobs throughout the United States.”

President Obama’s recognition of WFES comes on the heels of a visit this week from U.S. Secretary of State Hillary Clinton to Abu Dhabi where she toured the Masdar Institute of Science and Technology – a graduate level institution dedicated to innovations in clean energy and established in partnership with the Massachusetts Institute of Technology. She emphasized the strong relationship between the United States and the United Arab Emirates and also praised Abu Dhabi’s commitment to the development of renewable energy and climate change mitigation.

“I want my country to know how advanced you are in pursuing clean renewable energy. I want the world to know that the US is partnering with you because we are betting on Abu Dhabi and the UAE,” said Secretary of State Hillary Clinton.

“We are betting that this incredible investment represented by Masdar is going to pay off,” added Secretary Clinton. “And when it pays off, it will not only mean a better life for the people in this country and in this region, it will have ripple effects throughout the world.”

WFES received a further message of support from the US Ambassador to the United Arab Emirates, HE Richard G. Olson in the guide to exhibitors.

“I am pleased to lend my endorsement to the U.S. Department of Commerce’s recognition of the World Future Energy Summit that has evolved as the world’s foremost and must-attend annual meeting for the renewable energy and environment industry,” wrote Ambassador Olson.

Focusing on renewable and future energy solutions, innovations, investments, policy and vision, WFES will be held at Abu Dhabi National Exhibition Centre, ADNEC, from 17th to 20th January 2011 and expects more than 25,000 attendees from around the world. The Summit that will cover a wide range of themes including energy policy, investment and funding, green buildings, clean transport, solar, wind and biofuels.

No comments:

Post a Comment