Dini ni mfumo wa maishani

Dini ni mfumo wa maishani

Monday, August 1, 2011

Hivi sasa barabara mpya zinajengwa kwa ajili ya kombe la dunia 2014






Hivi sasa barabara mpya zinajengwa, viwanja vya ndege navyo vinaanza kupata sura mpya inayohitajika. Kumekuwa na kuchelewa kwa hapa na pale, lakini waandalizi hivi sasa wameonesha matumaini katika kazi za maandalizi. Na tofauti na uamuzi wa kuizawadia Qatar nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia la mwaka 2022, kwa Brazil kupata nafasi hiyo ya kuandaa, hakuna cha kutiliwa mashaka kwani kandanda ndio nyumbani kwake Brazil.


Tuangalie nchi za Afrika zilivyopangwa.

Mzunguko wa kwanza utakayo kuwa na mechi 12 za nyumbani na ugenini kati ya tarehe 11 hadi 15 mwezi wa Novemba, ambapo washindi watasonga mbele katika patashika za mzunguko wa pili.

Seychelles na Kenya

Guinea Bissau na Togo

Djibouti na Namibia

Mauritius na Liberia

Visiwa vya Comoro na Msumbiji

Equatorial Guinea na Madagascar

Somalia na Ethiopia

Lesotho na Burundi

Eritrea na Rwanda

Swaziland na jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo

Visiwa vya Sao Tome na Principe na Congo

Chad na Tanzania
- - -


Kwa makundi nchi hizo zimepangwa hivi:

Kundi A

Afrika Kusini
Botswana
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Somalia na Ethiopia
- - -

Kundi B

Tunisia, Visiwa vya Cape Verde, Sierra Leone, Equatorila Guinea na Madagascar


- - -
Kundi C
Ivory Coast
Morocco
Gambia
Chad/Tanzania
- - -
Kundi D
Ghana
Zambia
Sudan
Lesotho/Burundi
- - -
Kundi E
Burkina Faso
Gabon
Niger
Sao Tome and Principe/Congo
- - -
Kundi F
Nigeria
Malawi
Seychelles/ Kenya
Djibouti/Namibia
- - -
Kundi G
Egypt
Guinea
Zimbabwe
Comoros Islands/Msumbiji
- - -
Kundi H
Algeria
Mali
Benin
Eritrea/ Rwanda
- - -
Kundi I
Cameroon
Libya
Guinea Bissau/Togo
Swaziland/Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
- - -
Kundi J
Senegal
Uganda
Angola
Mauritius/Liberia

Mechi zitachezwa kati ya tarehe 1 mwezi wa Juni, 2012 na tarehe 10 mwezi wa Septemba 10, 2013.


Washindi wa kila kundi watasonga mbele hadi raundi ya tatu, wakicheza mechi za nyumbani na ugenini kati ya tareh 11 hadi 15 mwezi wa Oktoba, 2013 na washindi ndio watafuzu kucheza katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.











Muafaka kuhusu deni la marekani





Rais Barack Obama ametangaza kuwa viongozi wa chama cha Republican na chake cha Democratic wameafikiana kuhusu mpango wa kulipia deni la serikali.
Rais Obama

Marekani itapunguza matumizi yake kwa dola trilioni moja

Bw Obama amesema chini ya makubaliano hayo nchi hiyo itapunguza matumizi yake kwa dollar trilioni moja katika kipindi cha miaka kumi ijayo.

Hata hivyo mpango huo utapigiwa kura kwenye baraza za senate hii leo.

Muafaka huo umefikiwa ikiwa imebakia siku moja tuu kabla ya makataa ya kuongeza kiwango cha kukopa fedha za kulipia madeni yake.

Kwa wiki kadhaa, viongozi wa vyama hivyo wamekuwa wakivutana kuhusu njia bora ya kufuata kukabili madeni ya marekani.

Hali ambayo ilitishia kukwamihsa shughuli za serikali.

Baraza la senate lina hadi kesho kupiga kura kuongeza kiwango hicho cha kukopa hadi dola trilioni 14 lau sivyo shughuli za serikali zitakwama.

Rais Obama amesema kuwa mpango ulioafikiwa sio ule aliotarajia lakini amelazimika kuukubali ilikuwezesha huduma za serikali kuendelea na madeni yake yalipwe.

Utawala wa Rais Obama ulikuwa unakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa wapinzani kutoka chama cha Republican ambao walikuwa wanapinga pendekezo lake la kuwepo na mpango ambao utasitiri hali hadi mwisho wa mwaka ujao.

Chama cha Republicans kilitaka mpango huo uwepo hadi katikati ya mwaka ujao. Lakini sasa vyama hivyo vimekubaliana kuunda kamati maalum itakayotoa mapendekezo mapya mwezi Novemba.


















Bush Welcomes President-Elect Obama To White House




In This Photo: George W Bush, Michelle Obama, Barack Obama, Laura Bush
(AFP OUT) U.S. President George W. Bush (L) and Laura Bush (2nd-L) greet U.S. President-elect Barack Obama (R) and his wife Michelle Obama (2nd-R) on the South Portico of the White House November 10, 2008 in Washington, DC. This is the first visit for Barack Obama to the White House before he is sworn into office as President of the United States. First lady Laura Bush took soon to be first lady Michelle Obama on a tour of the White House as the President and Mr. Obama walked along the colonnade to the Oval Office where they will have a meeting. On January 20th Obama will be sworn in as the 44th president of the United States.



Michelle Obama, Laura Bush




In this handout image provided by the White House, First Lady Laura Bush (L) meets with U.S. President-elect Barack Obama's wife Michelle Obama in the private residence of the White House November 10, 2008 in Washington, DC. This is the first visit for Barack Obama to the White House before he is sworn into office as President of the United States. First lady Laura Bush took soon to be first lady Michelle Obama on a tour of the White House as the President and Mr. Obama walked along the colonnade to the Oval Office where they had a meeting. On January 20th Obama will be sworn in as the 44th president of the United States.







Rais Obama atofautiana na upinzani.







Rais Barack Obama

Rais Barack Obama amekuwa na kikao kilichokumbwa na mjala na maneno makali wakati wa kujadili nakisi ya bajeti ya kitaifa.

Mmoja wa wabunge wa upinzani aliyeshiriki kikao hicho ambacho kilikuwa cha nne na kushirikisha wabunge wa upinzani kutoka chama cha republican amenukuliwa akisema kwamba rais Obama alionekana mwenye kero na kuapa kutoridhia masharti ya upinzani na liwalo liwe.

Hata hivyo mmoja wa wabunge wa Democrats amesema taarifa kwamba rais aliondoka kwa ghathabu kutoka kikao hicho zilitiliwa chumvi.

Awali mmoja ya mashirika ya kutathmini viwango vya uchumi wa dunia ilionya dhidi ya uchumi wa Marekani kudorora zaidi ikiwa taifa halitatua nakisi ya bajeti inayokisiwa kufikia dola trilioni 14.











Bajeti ya Marekani imekwama







Mjadala kati ya wanasiasa, kuhusu bajeti, na jinsi ya kuzidisha kiwango cha mkopo wa serikali ya Marekani ungali umekwama.
Biramu linaloonesha deni la taifa nje ya ofisi ya kodi za mapato, Marekani.

Ufumbuzi unatakiwa ufikiwe kabla ya Jumaane, ambapo Wizara ya Fedha itaanza kupungukiwa na fedha za kulipia matumizi ya serikali.

Ijumaa usiku, baraza la wawakilishi, ambalo wabunge wake wengi ni kutoka chama cha Republican, lilipitisha mswada kuzidisha kiwango cha mkopo na kupunguza matumizi ya serikali, lakini mswada huo ulikataliwa na baraza la Senate, lenye wajumbe wengi wa chama cha Democrat.

Hali ya uhasama na mashindano imetanda Washington huku Jumaane inakaribia.

Wanasiasa bado wanavutana wakati wanahitaji kupatana ili kuepuka wasi-wasi na pengine matafaruku katika uchumi wa Marekani, ikiwa muafaka haukufikiwa kabla ya tarehe ya mwisho, yaani tarehe mbili Agosti.

Mswada uliopendekezwa na wabunge wa chama cha upinzani cha Republican Ijumaa, katika baraza la wawakilishi, ulizimwa katika baraza la Senate, ambako wajumbe wa chama cha Democrat sasa wanashindana na upinzani, na wanajaribu kusukuma mbele pendekezo lao wenyewe.

Lakini mswada huo piya, uliopendekezwa na kiranja wa chama cha Democrat, Harry Reid, unafanyiwa kazi ili ukubalike kwa wengi.

Vikao kati ya wanasiasa vitaendelea weekendi nzima na huenda makubaliano yakafikiwa dakika ya mwisho, na hatimaye kuwatuliza raia na masoko.










Kadi ya kupimia damu yavumbuliwa







Kibanzi kinaweza kupima virusi vya ukimwi

Utafiti mmoja wa kisayansi umesema, chombo ambacho ni rahisi kubebeka na chenye bei nafuu cha kupimia damu kinaweza kuleta mafanikio mapya katika kubaini ugonjwa hasa katika maeneo ya vijijini.

Kulingana na utafiti uliofanywa na jarida la Nature Medicine, chombo hicho kiitwacho mChip kina ukubwa wa kadi ya benki na huweza kutambua maradhi katika kipindi cha dakika chache tu.

Upimaji wa sampuli za awali za maradhi kama ukimwi na kaswende nchini Rwanda zilionyesha takriban asilimia 100 kuwa sahihi.

Kifaa hicho kilichotengenezwa Marekani kitagharibu dola moja ya kimarekani.

Gharama yake ni ndogo zaidi ukilinganisha na upimaji unaofanyika kwenye maabara ambao ndio unaotumika kwa sasa.

Kibanzi au chip hiyo ina maeneo 10 ya kutambua, na kinaweza kupima ugonjwa zaidi ya moja kwa damu kidogo tu inayotokana kwa kujichoma na sindano ndogo.

Majibu yanaweza kuonekana kwa macho tu au kwa chombo cha kutambua chenye bei nafuu.

Samuel Sia, Profesa kutoka chuo kikuu cha Columbia ambaye ndiye kiongozi wa uundwaji wa kibanzi hicho alisema, " Wazo kuu lilikuwa ni kuweza kupima maradhi mengi na iweze kuwafikia wagonjwa popote duniani, badala ya kuwalazimisha kwenda kwenye zahanati kutoa damu na kusuburi majibu kwa siku kadhaa."

Upimaji mwingi uliofanywa kwa sampuli za awali za kifaa hicho zilifanyika mjini Kigali, Rwanda.

Zilionyesha kuwa sahihi kwa asilimia 95 baada ya kupimwa kwa virusi vya ukimwi na sahihi kwa asilimia 76 baada ya kupima kaswende.

Watafiti wana matumaini ya kutumia mChip kujaribu kuongeza uwezekano wa kupima maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana kwa wajawazito, hasa barani Afrika.

Aina nyingine ya kibanzi hicho nacho kimeundwa kupima saratani ya kibofu.










Jeshi la Syria linashambulia Hamah








Jeshi la Syria limeshambulia kwa mizinga sehemu za mji wa Hamah, baada ya kuuzingira kwa miezi kadha.
Jeshi la Syria

Kwa mujibu wa wakaazi wa Hamah, watu kama 10 wameuwawa.

Taarifa nyengine zinasema waliouwawa ni kama 20.

Mji ambao umekuwa na maandamano makubwa zaidi nchini Syria sasa unashambuliwa.

Jeshi limeuzingira mji wa Hamah kwa miezi sasa, na leo alfajiri lilianza kuushambulia kwa mizinga.

Mkaazi mmoja wa Hamah anasema habari wanazopata kutoka hospitali ni kuwa watu wengi wameuwawa na kujeruhiwa.

Jeshi lilishambulia kutoka sehemu kadha, lakini kuna ripoti kuwa vifaru kama 16 vimeungana na upinzani.

Wanajiji walisherehekea hayo, lakini piya kuna khofu kuwa huo pengine ni mtego ili kuruhusu vifaru zaidi kuingizwa.

Inaonekana kuwa serikali inauogopa mji wa Hamah, kwa sababu ya mashambulio yaliyofanywa huko miaka ya '80, ambapo watu kama elfu 10 waliuliwa na jeshi la Rais Hafidh Assad, baba yake rais wa sasa.

Shambulio la leo linaonekana kama ujumbe kutoka kwa serikali, kuwa haitovumilia maandamano makubwa, hasa kabla ya mwezi wa Ramadan ambapo maandamano yanatarajiwa kuwa makubwa zaidi.

Lakini watu wametoka mabarabarani wakipiga kelele kuwa hawatokubali mauaji tena.









At least 95 people have been killed


At least 95 people have been killed after the army launched an attack on the flashpoint protest city of Hama in central Syria, a human rights activist has said.
A view shows the smoke rising in the city of Hama in this still image taken from video on Sunday.




A view shows the smoke rising in the city of Hama in this still image taken from video on Sunday. REUTERS photo

At least 95 people were killed on Sunday when the military launched an attack on the flashpoint protest city of Hama in central Syria, a human rights activist said.


Ammar Qorabi, who heads the National Organisation for Human Rights, reported the toll and also said army attacks across the country on Sunday killed at least 121 people and wounded dozens more.

Earlier, Rami Abdel Rahman of the Britain-based Syrian Observatory for Human Rights reported a death toll in Hama of 45, but said that number could rise because of the number of seriously wounded and a lack of medical supplies.

"The army and security forces entered Hama this morning and opened fire on civilians, killing 45 and wounding several more," Rami Abdel Rahman of the Britain-based Syrian Observatory for Human Rights said by telephone.

One Hama resident reached by phone told AFP that the army entered the city at around 6:00 am (0300 GMT).

Another said: "Five tanks are now deployed outside the governor's palace," and spoke of intermittent gunfire, while a third resident reported seeing four BTR-type armoured personnel carriers.

Elsewhere, "six people were killed and 50 wounded by security forces in the eastern city of Deir Ezzor and three were killed and dozens wounded at Harak in the southern Deraa region," Abdel Rahman said.

The oil hub of Deir Ezzor and Hama have been rallying points for pro-democracy protests since mid-March, while Hama has a bloody past.

In 1982, an estimated 20,000 people were killed in Hama when the army put down an Islamist revolt against the rule of President Bashar al-Assad's late father, Hafez.

The president replaced the governor of Hama after a record 500,000 protesters rallied in the opposition bastion on July 1 calling for the fall of the regime.

Activists said at the time it was the single largest demonstration of its kind since the pro-democracy movement erupted on March 15.

Since security forces gunned down 48 protesters in the city on June 3, Hama has escaped the clutches of the regime, activists say. The next day, more than 100,000 mourners were reported to have taken part in their funerals.

On Saturday, Abdel Rahman said troops shot dead three people who stoned a military convoy heading to quell growing anti-regime dissent in Deir Ezzor.

He said about 60 military vehicles including tanks, personnel carriers and trucks crammed with soldiers deployed in the city.

"The troops opened fire to frighten residents after reaching the governor's office," he said, quoting witnesses.

There were mounting fears the army was preparing to crack down on Deir Ezzor, increasingly at the forefront of anti-regime protests.

A man identifying himself as a Syrian army colonel told AFP in Nicosia that he had defected and has "hundreds" of troops under his command ready to confront the regular army in Deir Ezzor.

Riad al-Asaad warned the authorities against carrying out any operation in Deir Ezzor.

"I warn the Syrian authorities that I will send my troops to fight with the (regular) army if they do not stop the operations in Deir Ezzor," Asaad said.

"I am the commander of the Syrian Free Army," he said, adding that he commanded "hundreds" of troops and was calling from inside Syria "near the Turkish border."

His claim could not be independently verified.

Deir Ezzor, the main oil- and gas-producing region in Syria, which produces 380,000 barrels of oil per day, has seen almost daily demonstrations against the regime.

Meanwhile an opposition figure who declined to be named told AFP that 15 conscripts broke ranks from the troops who entered the central city of Homs on Saturday and fled.

"They have sought protection with residents," the source said.

On Friday, at least three people were killed in Deir Ezzor when security forces opened fire on 300,000 mourners at the funerals of three people killed the previous day, according to activists.

A total of 20 people were killed and 35 wounded on Friday across Syria as hundreds of thousands of demonstrators held anti-regime protests, rights groups said.

Syrian opposition figures meeting in Algeria on Saturday spoke out against any foreign intervention as the bloody crackdown continued.

"We refuse all foreign intervention, we refuse to carry weapons," said Adnane el-Bouch, a Syrian lawyer living in Algeria, during a meeting of a Syrian support committee at Amnesty International premises.

"It's a peaceful revolution... our weapons are cameras and mobile phones."

Since anti-regime protests broke out, the crackdown on dissent has resulted in the deaths of more than 1,500 civilians and more than 360 members of the security forces, according to a Syrian Observatory toll.

More than 12,000 people are also reported to have been arrested in the crackdown, and thousands of others have fled the country, rights groups say.










Soko kuu lateketea Kampala







Moto Kampala

Wachuuzi kama elfu kumi katika soko kuu la Owino mjini Kampala, wamepoteza mali zao zilizoteketea kwenye moto uliotokea Jumapili alfajiri.

Hii ni mara ya pili moto kutokea hapo katika kipindi cha miaka miwili.

Polisi walisema wanachunguza tukio hilo.

Salim Uhuru diwani wa mtaa huo alisema "hii ni mara ya pili soko limeshika moto. Ripoti ya polisi ya kwanza bado haijatoka na sasa moto umetokea mara ya pili. Hatujui kama moto umetokana na stima, au walichoma au jambo la kawaida. Hatujui."

"Lakini tunaomba wachuuzi warudi sokoni kwa sababu habari tulizopata ni kuwa watu wameshanunua ardhi hii. Na wakinunua ardhi hii, kutufukuza wanachochoma vitu vya watu," aliongeza.

"Lakini sisi kama madiwani wa eneo hili, tumewaambia wachuuzi warudi katika maduka yao. Hakuna mtu aliyewahi kuokoa mali yake. Yote imeungua."











Umoja wa Afrika kujadili Somalia








Somalia ukame

Umoja wa Afrika umetangaza kuwa utafanya mkutano wa viongozi ili kuchanga msaada kwa watu wa Somalia walioathirika na ukame.

Taarifa hiyo imetolewa baada ya malamiko kadha katika vyombo vya habari vya Afrika, kwamba viongozi wa Afrika wameshindwa kuwasaidia Wasomali wanaokabili njaa.

Makamo Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Bwana Mwencha alitoa tangazo la mkutano, wakati akizuru kikosi cha usalama cha umoja huo mjini Mogadishu.

Umoja wa Mataifa unasema watu milioni 12 wanahitaji msaada wa haraka katika eneo hilo.









Boko Haram kuzungumza na serikali Nigeria











Serikali ya Nigeria imetangaza kwamba inataraji kufanya mazungumzo na kikundi cha waislamu wenye siasa kali, cha Boko Haram.

Kamati imeteuliwa kuchunguza mtafaruku katika eneo la kaskazini-mashariki mwa nchi, baada ya watu kadha kuuwawa katika mapambano ya karibuni baina ya Boko Haram na jeshi.

Kamati hiyo ya wajumbe 10 imepewa kama wiki mbili kutoa mapendekezo.

Kamati imeagizwa kutazama swala la usalama katika eneo la ghasia la kaskazini-mashariki, na kuanza mazungumzo na kikundi cha Boko Haram, cha Waislamu wa msimamo mkali.

Hivi karibuni wapiganaji wa kikundi hicho, wamefanya mashambulio kadha, hasa dhidi ya askari wa usalama.

Wanajeshi wamezidishwa huko, na wengine wamelipiza kisasi, na wakati mwengine kuuwa raia.

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, anapenda kusema kuwa sera yake ni kuuma na kupuliza.

Lakini hadi sasa kuuma sana kumezidi kuharibu mambo; huku maelfu wamelihama eneo.

Mfano ambao rais anataka kujaribu tena ni ule uliotumiwa katika eneo la Niger Delta; ambako baada msamaha wa serikali, pamoja na fidia kubwa kwa wapiganaji, eneo hilo sasa ni shuwari.

Hadi sasa, Boko Haram hawakuonesha ishara kuwa wanataka kuzungumza.

Siku za nyuma walishikilia kuwa jeshi lazima liondoke kwanza, kabla ya mazungumzo kuanza.










INTERVIEW OF BOKO HARAM SUPREME LEADER USTAZ MOHAMMED YUSUF
Boko Haram is an Islamic radical and militant group operating in North and Central Nigeria, on the demographic border region between the Muslims in Nigeria, living mainly in Northern Nigeria and the Christian inhabiting mainly the South of the country. The term "Boko Haram" comes from the Hausa word BOKO meaning "Western or non-Islamic education" and the Arabic word HARAM meaning "sin".
Boko Haram was founded in 2002 in Maiduguri, central Nigeria, by Ustaz Mohammed Yusuf. In 2004 it moved to Kanamma, Yobe State of Nigeria, on the far North-East in the edge of the Sahara desert on the border with Niger where other Islamic militant groups like MAGHREB al-Qaeda are operating too. In Kanamma Boko Haram set up a base called "Afghanistan", used to attack nearby police outposts, killing police officers. Ustaz Mohammed Yusuf is hostile to democracy and the secular education system, vowing that "this war that is yet to start would continue for long" if the political and educational system was not changed. Ustaz Mohammed Yusuf himself was killed by Nigerian troops on 07/31/2009 (see - Bauchi 07.26.09).
Boko Haram includes members who come from neighboring Chad and speak only in Arabic and not one of the Local Nigerian languages to demonstrate their loyalty to the Islamic Kuraan. In a 2009 BBC interview, Yusuf stated that the belief that the world is a sphere contrary to Islam and should be rejected, along with Darainism and the theory that rain comes from water evaporated by the sun.

Incase you missed the interview of Boko Haram SUPREME LEADER USTAZ MOHAMMED YUSUF during interrogation by Nigeria's SSS(State Security Service) here is a transcript of the interview.








Bahrami amsamehe aliyempofua





Ameneh Bahrami



Mwanamke wa Iran ambaye alipofoka aliposhambuliwa kwa tindi kali, amemsamehe mwanamme aliyemshambulia, saa chache tu kabla ya mfungwa huyo akitarajiwa naye kupofolewa, kama adhabu yake.

Majid Movahedi alikutikana na makosa ya kumrushia tindi kali usoni Ameneh Bahrami, baada ya bibi huyo kukataa posa yake mara kadha.

Baada ya hukumu kutolewa, Ameneh Bahrami alisema yeye mwenyewe atamimina tindi kali kwenye macho ya Bwana Movahed.

Mashirika ya kupigania haki za kibinaadamu yalilalamika juu ya hukumu hiyo.

Bi Bahrami sasa ameliambia shirika la habari la Iran, kwamba, ingawa Mungu anataja adhabu ya malipo, lakini piya anasema kuwa kumsamehe mkosa ni muhimu zaidi.

Bi Bahrami anadai fidia kwa majaraha yake.












Man United yailaza Barcelona 2-1




Bao la ushindi alilofunga Michael Owen dakika ya 76 liliiwezesha Manchester United kuwalaza mabingwa soka wa bara la Ulaya Barcelona 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa kwa patashika za Ligi Kuu, uliofanyika mjini Washington DC.


Michael Owen baada ya kufunga bao la ushindi

Mbele ya mashabiki karibu 82,000, Nani alitangulia kuipatia Manchester United bao la kuongoza katika dakika ya 22.

Barcelona, ikicheza bila ya Lionel Messi, ilisawazisha katika dakika ya 70 kwa mkwaju wa Thiago Alcantara.

Owen alimiminiwa pande la Tom Cleverley na kupachika bao la ushindi wakati United wakikamilisha ziara ya Amerika Kaskazini na kushinda mechi zake zote tano ilizocheza.

Owen aliandika katika mtandao wa kijamii wa tweeter baada ya mchezo huo: "Kama ilivyo kawaida ya Barca, upande wa upinzani unapata shida sana kumiliki mpira! Na ndivyo ilivyokuwa katika mchezo wa leo! Nashukuru nimefanikiwa kufunga bao."

United walifungwa na Barcelona katika fainali ya Kombe la Ubingwa wa Ulaya katika uwanja wa Wembley mwezi wa Mei, ilionekana mabingwa hao wa soka wa England wakipata nafasi ndogo ya kulipiza kisasi.

Kikosi hicho cha Sir Alex Ferguson kitarejea nyumbani kujiandaa kwa mchezo wa kuwania Ngao ya Jumuia dhidi ya washindi wa Kombe la FA, Manchester City siku ya Jumapili ijayo katika uwanja wa Wembley.

Meneja msaidizi wa Manchester United Mike Phelan alisema: "Mechi ya usiku huu haikuwa ya kuwania kitu chochote. Ilikuwa muhimu kwamba wachezaji tuliowapanga walikuwa wanaelewa nini kinachohitajika unapopambana na timu bora duniani.

Pamoja na Messi kutocheza, Barcelona iliamua kutomchezesha Xavi, Carlos Puyol na Gerard Pique katika kikosi chao kilichoanza.








Watu 11 wauwawa katika ghasia Uchina






Xinjiang China





Vyombo vya habari vya Uchina vinasema kuwa watu 11 wameuwawa katika kisa cha pili cha ghasia katika majuma mawili, kwenye jimbo la magharibi la Xinjiang.

Shirika la habari la taifa, Xinhua, lilisema watu wanane walikufa jana usiku katika mji wa Kashgar, wakati wanaume wawili walipoliteka lori na kuwapiga visu wapita njia.

Kabla ya shambulio hilo, kulitokea miripuko miwili.

Xinhua imeripoti kuwa leo piya kulitokea mripuko mwengine, uliouwa watu watatu.

Kulitokea ghasia za kikabila katika jimbo la Xinjiang, miaka miwili iliyopita, kati ya watu wa kabila la Uighur, ambao ni Waislamu, na ni wachache, na wanachukia utawala wa Beijing.

Wa-Uighur wanaoishi uhamishoni, wanasema kulikuwa na amri ya kafyu huko Kashgar, na watu kama mia-moja wamekamatwa.












Kasumba inapitia Afrika Mashariki







Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wanaofanya magendo ya mihadarati Afrika sasa wanapitia Afrika Mashariki,
kwa sababu ya vikwazo vingi Asia na Mashariki ya Kati, na hivo kuleta uvunjaji wa sheria na matumizi zaidi ya mihadarati katika eneo hilo la Afrika Mashariki.

Inakisiwa kuwa biashara ya mihadarati ilifika dola bilioni 68 dunia nzima, katika mwaka wa 2009.

Ofisi ya Kupambana na Mihadarati na Uhalifu ya Umoja wa Mataifa, inasema ina wasiwasi kuwa Afrika Mashariki imekuwa njia inayotumiwa na wafanya magendo, kwa sababu kanda hiyo haina uwezo wa kupambana na magendo na uraibu wa mihadarati.

Inasema madawa ya kulevya na idadi ya walanguzi waliokamatwa, inaonesha kuwa wafanya magendo hayo, hasa magengi kutoka Afrika Magharibi, wanazidi kusafirisha kasumba kutoka Afghanistan na Pakistan kupitia Afrika Mashariki, kisha kupeleka Ulaya na kwengineko.

Afghanistan ndio mzalishaji mkubwa kabisa wa kasumba, na asilimia 40 hupitishwa Pakistan, kabla ya kuelekezwa kwengineko.

Ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa inasema katika miezi mitatu ya mwanzo ya mwaka huu, shehena mbili za kasumba, kila moja zaidi ya kilo mia moja, zimeripotiwa Kenya na Tanzania.

Inaeleza kuwa sababu ya magendo hayo kuzidi ni rushwa, umaskini na uwezo haba wa idara za kuweka sheria

No comments:

Post a Comment